Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imeanza kutumia dawa ya majaribio aina ya mAb114 kutibu mlipuko wa karibuni wa homa hiyo inayosababishwa na virusi.
Shirika la Afya Duniani WHO limesema, hali mpya ya maambukizi ya ugonjwa wa Ebola nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo DRC inazilazimisha nchi za jirani kuchukua hatua za tahadhari ili kuzuia ungojwa huo hatari kuenea.
Watu wasiopungua 33 wanaripotiwa kufariki dunia kwa ugonjwa wa Ebola mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, siku chache baada ya maambukizi ya ugonjwa huo hatari kuripotiwa tena nchini humo.
Shirika la Afya Duniani WHO, limesema litafanya kila liwezalo kudhibiti kuenea kwa mlipuko wa Ebola ambao umethibitishwa huko jimbo la Kivu Kaskazini nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.
Serikali ya Sierra Leone imetangaza habari ya kungunduliwa virusi vipya ya ugonjwa hatari wa Ebola, miaka miwili baada ya maradhi hayo kusemekana kuwa yamemalizika kabisa nchini humo.
Shirika la Afya Duniani WHO limetangaza kuwa limepunguza kiwango cha tishio la kutokea kwa ugonjwa wa Ebola nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Kongo kutoka kiwango cha juu hadi kiwango cha wastani katika ngazi ya kitaifa na kimataifa.
Wanasiasa nchini Uganda wameonywa kuhusu kutoa matamshi yanayoweza kuzusha hofu na wasiwasi mkubwa nchini Uganda na katika ukanda mzima wa Afrika Mashariki kuhusu ugonjwa hatari wa Ebola. Mwandishi wetu Kigozi Ismail ametutayarishia ripoti maalumu kuhusu suala hilo...
Serikali ya Uganda imekanusha taarifa zilizoenea za kuibuka nchini humo ugonjwa hatari wa Ebola ambao umeua makumi ya watu katika nchi jirani ya Jamhuri ya Kidemokarasia ya Kongo.
Wizara ya Afya katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo leo Jumatatu inaaza kupeana chanjo ya ugonjwa hatari wa Ebola katika vijiji viwili vilivyoathiriwa na mlipuko wa sasa wa maradhi hayo.
Wagonjwa watatu walioambukizwa ugonjwa hatari wa Ebola wametoroka eneo la karantini walimokuwa katika hospitali moja huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo katika mji wa Mbandaka huku madakatari wakiwa mbioni kuzuia ugonjwa huo hatari kuenea.