-
Zaidi ya watu 800,000 wamekuwa wakimbizi kutokana na ukame huko Ethiopia na Somalia
Mar 10, 2022 00:41Msemaji wa Umoja wa Mataifa ametangaza kuwa, ukame na uhaba wa chakula umewafanya watu zaidi ya 845,000 kuwa wakimbizi huko Ethiopia na Somalia.
-
Naibu Katibu Mkuu wa UN: "Jinai zisizoweza kufikirika" zimefanyika Ethiopia hasa dhidi ya wanawake
Feb 13, 2022 00:44Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani kile alichokielezea kuwa ni jinai zisizoweza kufikirika zilizofanywa nchini Ethiopia, hasa dhidi ya wanawake na kutaka haki itendeke kwa waliofanyiwa jinai hizo.
-
Kufutiwa utawala ghasibu wa Israel hadhi ya mwanachama mtazamaji katika Umoja wa Afrika
Feb 08, 2022 05:28Mkutano wa 35 wa wakuu wa Umoja wa Afrika (AU) uliofanyika tarehe 5 na 6 za mwezi huu wa Februari huko Addis Ababa Ethiopia umesitisha hadhi ya utawala ghasibu wa Israel ya kuwa mwanachama mtazamaji katika umoja huo.
-
FAO yatoa wito wa kuwasaidia waathirika wa ukame katika nchi za Kenya, Ethiopia na Somalia
Feb 04, 2022 04:23Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo FAO katika Ukanda wa Afrika Mashariki limetoa wito kwa wananchi, taasisi binafsi na mashirika ya dini kuchangia wananchi walioathirika na ukame pamoja na mazao yao kuharibiwa na nzige katika nchi za Kenya, Ethiopia na Somalia.
-
Waasi nchini Ethiopia watishia kuanzisha tena mapigano katika eneo la Afar
Jan 26, 2022 23:07Waasi wa Harakati ya Ukombozi ya Watu wa Tigray wa (TPLF) katika eneo hilo la kaskazini mwa Ethiopia, wamesema wamechokozwa na hivyo wataanzisha operesheni katika jimbo jirani la Afar, hali inayorudisha nyuma matumaini ya kumaliza mzozo huo unaoendelea kwa mwezi wa 14 sasa.
-
Msafara wa misaada ya kibinadamu kuelekea Tigray wazuiwa
Jan 26, 2022 00:43Duru zinazohusika na masuala ya kibinadamu nchini Ethiopia zimeripoti kuwa msafara wa misaada ya kibiandamu iliyokuwa ikipelekwa Tigray kaskazini mwa Ethiopia imezuiliwa.
-
Afisa mmoja wa ngazi za juu wa kijeshi wa Sudan atembelea Ethiopia
Jan 22, 2022 10:32Afisa mmoja wa ngazi a juu wa Sudan ametembelea nchi jirani ya Ethiopia wakati huu ambapo nchi hizo mbili zina mzozo mkubwa wa mpaka.
-
UN: Hujuma za anga Tigray zimeua raia 108 wa Ethiopia
Jan 14, 2022 21:19Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, kwa akali raia 108 wameuawa tangu mwanzoni mwa mwezi huu wa Januari hadi sasa, katika mashambulizi ya anga katika eneo la Tigray la kaskazini mwa Ethiopia.
-
Vita vya Ethiopia na jitihada za kutatua mgogoro wa nchi hiyo
Jan 13, 2022 00:51Wakati maafisa wa serikali ya Ethiopia wakiahidi kuanzisha mazungumzo ya kitaifa nchini humo, Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Tigray (TPLF) imetangaza kuwa mashambulizi ya jeshi la Ethiopia katika eneo hilo yamesababisha vifo vya zaidi ya raia 56.
-
UNICEF: Pande zinazozozana Tigray Ethiopia zimefanya ukandamizaji dhidi ya watoto
Jan 10, 2022 10:16Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umezituhumu pande zinazopigana katika jimbo la Tigray la kaskazini mwa Ethiopia kwamba, zimefanya ukandamizaji mkubwa dhidi ya watoto.