-
UN: Hujuma za anga Tigray zimeua raia 108 wa Ethiopia
Jan 14, 2022 21:19Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, kwa akali raia 108 wameuawa tangu mwanzoni mwa mwezi huu wa Januari hadi sasa, katika mashambulizi ya anga katika eneo la Tigray la kaskazini mwa Ethiopia.
-
Vita vya Ethiopia na jitihada za kutatua mgogoro wa nchi hiyo
Jan 13, 2022 00:51Wakati maafisa wa serikali ya Ethiopia wakiahidi kuanzisha mazungumzo ya kitaifa nchini humo, Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Tigray (TPLF) imetangaza kuwa mashambulizi ya jeshi la Ethiopia katika eneo hilo yamesababisha vifo vya zaidi ya raia 56.
-
UNICEF: Pande zinazozozana Tigray Ethiopia zimefanya ukandamizaji dhidi ya watoto
Jan 10, 2022 10:16Mfuko wa Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umezituhumu pande zinazopigana katika jimbo la Tigray la kaskazini mwa Ethiopia kwamba, zimefanya ukandamizaji mkubwa dhidi ya watoto.
-
Kuachiliwa huru wapinzani wa serikali ya Ethiopia; juhudi za kuanzisha mazungumzo ya kitaifa
Jan 09, 2022 23:21Baada ya miezi kadhaa ya mzozo na vita nchini Ethiopia, Abiy Ahmed Waziri Mkuu wa nchi hiyo ametangaza msamaha na kuwaachia huru wafungwa mashuhuri wa kisiasa akiwemo kiongozi wa upinzani Jawar Mohammed na maafisa wa chama cha upinzani cha Tigray na hivyo kupiga hatua ya kwanza kwa minajili ya kurejesha utilivu wa kisiasa na kuandaa uwanja kwa ajili ya mazungumzo ya kitaifa.
-
Shambulizi ya anga laua wafanyakazi 56 wa misaada ya kibinadamu Tigray
Jan 09, 2022 01:16Shambulio la anga katika eneo la Tigray nchini Ethiopia limesababisha vifo vya watu 56 na kujeruhi wengine 30 wakiwemo watoto, katika kambi ya watu waliokimbia makazi yao. Hayo yamesemwa na wafanyakazi wawili wa kutoa misaada wakinukuu mamlaka za eneo hilo na watu walioshuhidia maafa hayo.
-
Ethiopia yatangaza msamaha kwa wafungwa wa kisiasa akiwemo kiongozi wa upinzani
Jan 08, 2022 03:40Serikali ya Ethiopia imetangaza kuwa itatoa msamaha na kuwaachia huru wafungwa mashuhuri wa kisiasa akiwemo kiongozi wa upinzani Jawar Mohammed na maafisa wa chama cha upinzani cha Tigray.
-
Katibu Mkuu wa UN akaribisha hatua chanya zilizochukuliwa na pande zinazopigana nchini Ethiopia
Dec 25, 2021 09:39Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amekaribisha tangazo la serikali ya Ethiopia kwamba jeshi lake litasitisha mashambulizi katika eneo ambako liko hivi sasa.
-
Ethiopia: Hatuna nia ya kuwashambulia waasi wa Tigray
Dec 22, 2021 09:39Serikali ya Ethiopia imetangaza kuwa, haina nia ya kuendeleza mashambulizi dhidi ya waasi wa Harakati ya Ukombozi wa Watu wa Tigray (TPLF).
-
Waasi wa Tigray warudi nyuma na kuondoka maeneo waliyokuwa wakiyadhibiti
Dec 20, 2021 23:05Mkuu wa Harakati ya Ukombozi ya Watu wa Tigray (TPLF) ametangaza kuwa, wapiganaji wa harakati hiyo wamerudi nyumana kuondoka katika maeneo yote nje ya eneo la Tigray huko kaskazini mwa Ethiopia ikiwa ni katika kujibu maombi ya kimataifa na kutoa fursa ya kurejesha amani katika eneo hilo.
-
Ethiopia: Baraza la Haki za Binadamu la UN linatumika kisiasa
Dec 18, 2021 00:04Ethiopia imekosoa kufanyika kwa kikao maalumu cha Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa kujadili na kutathmini visa vya ukiukaji wa haki za binadamu nchini humo kufuatia mzozo unaoendelea kati ya serikali na waasi wa Tigray.