-
Palestina: Kwa siku 108, Israel imeua watoto 11,000 na wanawake 7,500 Gaza
Jan 23, 2024 03:08Mamlaka za Palestina zimetangaza kuwa, jeshi vamizi la utawala wa Kizayuni wa Israel limeua watoto 11,000 na wanawake 7,500 katika Ukanda wa Gaza na kuongeza kuwa jeshi hilo katili limedondosha zaidi ya tani 65,000 za mada za miripuko katika vita vya upande mmoja lilivyoanzisha dhidi ya Wapalestina waliowekewa mzingiro.
-
HAMAS: Wapalestina 500,000 wa Gaza wapo katika hatari ya kufa njaa
Jan 22, 2024 23:40Afisa mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema zaidi ya watu nusu milioni wakazi wa Ukanda wa Gaza wapo katika hatari ya kufa njaa kutokana na taathira hasi za vita vya mauaji ya kimbari vya utawala wa Israel dhidi ya Wapalestina wa eneo hilo lililozingirwa.
-
Kesi iliyofunguliwa na A/Kusini dhidi ya Israel yaendelea kuungwa mkono
Jan 21, 2024 23:28Kwa mara nyingine tena, Ubelgiji imejiunga kwenye safu ndefu ya waungaji mkono wa hatua ya Afrika ya Kusini ya kufungua kesi dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki ICJ kutokana na jinai zake za kupindukia dhidi ya watoto wachanga, wanawake, vizee na watu wa kawaida huko Ghaza.
-
Waliouawa shahidi Gaza wapindukia 25,000, Israel yaendeleza mashambulizi ya kinyama
Jan 21, 2024 10:09Maafisa wa Palestina katika Ukanda wa Gaza wametangaza kuwa, wakati vita angamizi vilivyoanzishwa na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Gaza vimeingia katika siku yake ya 107 leo, hadi sasa Wapalestina 25,105 wameshauawa shahidi na 62,681 wamejeruhiwa.
-
Sayyid Nasrullah: Gaza ni nembo ya umoja wa damu, silaha, medani na lengo la Umma wa Kiislamu
Jan 20, 2024 23:10Katibu Mkuu wa harakati ya Hizbullah ya Lebanon, Sayyid Hassan Nasrullah ametuma ujumbe katika Mkutano wa 12 wa Kimataifa wa "Gaza; Nembo ya Muqawama" na kusisitiza kuwa Gaza leo hii ni nembo ya umoja wa damu, silaha, medani na lengo la Umma wa Kiislamu.
-
Wananchi Uingereza waendeleza maandamano ya kuiunga mkono Gaza
Jan 20, 2024 23:09Maelfu ya watu nchini Uingereza kwa siku ya 15 mtawalia wamemiminika katika miji mbalimbali ya nchi hiyo kulaani na kupinga jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya Gaza.
-
Baada ya kubanwa kila upande Israel, sasa Umoja wa Ulaya waomba kusimamishwa vita Ghaza
Jan 19, 2024 04:40Baada ya utawala wa Kizayuni kubanwa kila upande, kutokea Ghaza hadi kwenye mipaka ya Lebanon na kutokea Iraq hadi Yemen na Bahari Nyekundu, sasa Umoja wa Ulaya umetaka kusimamishwa vita kikamilifu katika Ukanda wa Ghaza na hii ikiwa ni mara ya kwanza kwa umoja huo unaoiunga mkono kikamilifu Israel, kuomba jambo kama hilo.
-
Sababu za vita vya Gaza kuendelea kwa muda mrefu
Jan 17, 2024 01:03Licha ya kupita siku 100 tangu vita vya utawala wa Kizayuni dhidi ya Ukanda wa Gaza vianze, lakini bado hakuna matarajio ya kumalizika kwa vita hivyo.
-
Kuanza kusikilizwa mashtaka ya Afrika Kusini katika Mahakama ya Kimataifa ya Haki dhidi ya utawala wa Kizayuni
Jan 11, 2024 23:11Mahakama ya Kimataifa ya Haki yenye makao makuu yake mjini The Hague Uholanzi Alhamisi na Ijumaa inasikiliza na kukusanya mitazamo ya kisheria ya Afrika Kusini na utawala wa Kizayuni kuhusu kesi ya mauaji ya kimbari katika Ukanda wa Gaza. Moja ya shughuli za mahakama hiyo ni kushughulikia mashtaka yanayohusiana na Mkataba wa Mauaji ya Kimbari wa 1948. Mkataba huo unatambuliwa rasmi na nchi 153.
-
Umoja wa Mataifa: Vita vya Gaza lazima vikomeshwe
Jan 07, 2024 07:44Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na Masuala ya Kibinadamu Martin Griffiths amesema ni lazima Jamii ya Kimataifa itumie "ushawishi wake wote" kumaliza vita katika Ukanda wa Gaza.