-
Israel yakiri kuhusu nguvu ya Hizbullah ya Lebanon
Mar 05, 2016 03:05Utawala wa Kizayuni wa Israel umekiri kuhusu uwezo wa kijeshi wa Harakati ya Hizbullah ya Lebanon.
-
Watunisia walaani uamuzi wa [P]GCC wa kuitaja Hizbullah kuwa kundi la kigaidi
Mar 04, 2016 07:49Washindi wa tunzo ya amani ya Nobel kutoka Tunisia wamelaani hatua ya baadhi ya nchi za Kiarabu ya kuiweka Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon katika orodha ya makundi ya kigaidi.
-
Saudia yaendelea kushirikiana na utawala wa Kizayuni wa Israel
Mar 04, 2016 02:46Kufuatia kuongezeka wasiwasi kuhusu kuimarika ushawishi wa Iran katika eneo baada ya kutiwa saini mapatano ya nyuklia, Israel na Saudia zimezidi kukurubiana ili kukabiliana na hali hiyo.
-
Iran yapinga vikali taarifa ya GCC
Mar 03, 2016 14:30Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani vikali taarifa iliyotolewa na Baraza la Ushirikiano wa Ghuba ya Uajemi inaliyoitambua harakatri ya Hizbullah ya Lebanon kuwa ni kundi la kigaidi.
-
Algeria yapinga kutolewa tuhuma za ugaidi dhidi ya Hizbullah ya Lebanon
Mar 03, 2016 07:58Wizara ya Mambo ya Ndani ya Algeria Algeria imepinga kutolewa taarifa ya Mawaziri wa Mambo ya Ndani wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu dhidi ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Hizbullah ya Lebanon.
-
Abdulahiyan: Kuiita Hizbullah kuwa ni kundi la kigaidi hakuna maskahi kwa M. ya Kati
Mar 03, 2016 06:48Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa hatua ya kuiweka harakati ya Huzbullah ya Lebanon katika orodha ya makundi ya kigaidi ni sawa na kufumbia macho jinai zinazofanywa na utawala ghasibu wa Israel suala ambalo halina faida kwa usalama na amani na eneo la Mashariki ya Kati.
-
PGCC: Hizbullah ni taasisi ya kigaidi
Mar 03, 2016 03:10Nchi sita wanachama wa Baraza la Ushirikiano la Ghuba ya Uajemi zimeiweka Harakati ya Muqawama ya Lebanon Hizbullah ambayo inaendesha mapambano dhidi ya utawala ghasibu wa Kizayuni na magaidi huko Syria katika orodha eti ya magaidi.
-
Marekani, Israel, Saudia zinachochea fitna Mashariki ya Kati
Mar 02, 2016 02:50Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema kuwa, Marekani, utawala wa Kizayuni wa Israel na Saudi Arabia zinachochea fitna na mizozo ya kimadhehebu katika eneo nyeti la Mashariki ya Kati.
-
Hizbullah: Hatuwezi kuiomba Saudia msamaha
Feb 28, 2016 08:03Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Lebanon Hizbullah imeukosoa utawala wa Saudi Arabia kwa kula njama ya kuitumbukiza Lebanon katika mzozo wa ndani na kuongeza kuwa katu haiwezi kuiomba msahama serikali ya Riyadh kwa kusema ukweli.
-
'Sudan inaiuzia Saudia habari za kipelelezi kuhusu Hizbullah'
Feb 28, 2016 02:26Gazeti la al Akbar la Lebanon limeripoti kuwa, serikali ya Sudan inaiuzia Saudi Arabia habari za kipelelezi kuhusu mbinu zinazotumiwa na Hizbullah katika masuala mbalimbali hususan mbinu za harakati hiyo ya Kiislamu za kupambana na utawala ghasibu wa Israel.