-
Imarati yamtimua balozi wake wa Ethiopia kwa kushindwa kuandaa safari ya mkuu wake
Apr 20, 2018 14:08Serikali ya Imarati imemrejesha nyumba na kumpiga kalamu nyekundu balozi wake nchini Ethiopia.
-
Wanawake wahajiri wa Kiafrika wanadhalilishwa kingono katika jela zinazosimamiwa na Saudia na UAE, Aden
Apr 19, 2018 07:51Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch na Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi UNHCR yameripoti kuwa wanawake wahajiri wa Kiafrika wanakashifiwa na kudhalilishwa kingono katika mji wa Aden kusini mwa Yemen ambao unadhibitiwa na vikosi vya Imarati (UAE) na Saudi Arabia.
-
HRW: Mamluki wa Imarati wanawabaka wahajiri wa Kiafrika Yemen
Apr 18, 2018 07:38Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema mamluki wanaofadhiliwa na kuungwa mkono na Umoja wa Falme za Kiarabu nchini Yemen wanawabaka na kuwalawiti wahajiri wa kike na kiume raia wa Afrika katika nchi hiyo masikini ya Kiarabu.
-
Mgogoro kati ya Somalia na Imarati washtadi, Abu Dhabi yafunga hospitali yake Mogadishu
Apr 17, 2018 14:10Mgogoro kati ya Somalia na Imarati umezidi kushtadi ambapo mara hii serikali ya Abu Dhabi imechukua hatua ya kufunga hospitali yake mjini Mogadishu, mji mkuu wa Somalia.
-
Saudia na Imarati zawafanya mamluki maelfu ya vijana wa Afrika
Apr 17, 2018 14:03Gazeti la al-Quds al-Arabi limeripoti kuwa, Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu zinataka kuwasajili maelfu ya vijana wa Kiafrika zitakaowatumia katika operesheni zao za nje ya nchi vikiwemo vita dhidi ya Yemen.
-
Serikali ya Somalia yapinga kuingiliwa katika masuala yake ya ndani
Apr 17, 2018 08:05Rais Mohamed Abdullahi Mohamed wa Somalia amesema kuwa, serikali na wananchi wa nchi hiyo wanapinga uingiliaji wa madola ya kigeni katika masuala ya ndani ya nchi hiyo
-
Uhusiano wa Somalia na Umoja wa Falme za Kiarabu wazidi kuzorota
Apr 15, 2018 16:43Mzozo katika uhusiano baina ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) na Somalia umezidi kuzorota kutokana na hatua ya Imarati kuingilia mambo ya ndano ya nchi hiyo.
-
Somalia yaitaka UN kusitisha uvamizi wa Imarati Somaliland
Mar 29, 2018 04:34Mwakilishi wa Somalia katika Umoja wa Mataifa amelaani hatua ya Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) ya kukiuka maazimio ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa na ametaka hatua za lazima zichukuliwe ili kusitisha uchokozi huo wa Imarati.
-
Aghalabu ya wananchi wa Ufaransa wanataka nchi yao iache kuiuzia silaha Saudia
Mar 26, 2018 15:01Uchunguzi wa maoni uliofanywa hivi karibuni umeonyesha kuwa asilimia 75 ya wananchi wa Ufaransa wanataka nchi yao isimamishe uuzaji wa silaha kwa Saudi Arabia, Imarati na nchi nyingine zinaoendesha vita haribifu huko Yemen.
-
Qatar: Imarati imetutaka kuachana na maandalizi ya Kombe la Dunia 2022 ili iache kutuzingira
Mar 24, 2018 14:46Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Qatar amefichua kwamba, nchi nne zinazoizingira nchi hiyo zikiongozwa na Saudi Arabia, zimetoa sharti zito kwa Doha kwamba, inatakiwa kuchagua moja ya mambo mawili, ima kuachana na maandalizi ya michuano ya kombe la dunia 2022, au kuendelea kuzingirwa na nchi hizo.