-
Imarati yadai kuhusika katika kuuzuliwa Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani
Mar 14, 2018 14:31Abdulkhaliq Abdullah Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Umoja wa Falme za Kiarabu Imarati na ambaye pia ni Naibu wa Sheikh Mohammed bin Zayed Al Nahyan mrithi wa Mtawala wa Abu Dhabi amedai kuwa nchi hiyo imehusika katika kuuzuliwa Rex Tillerson Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani na kusema kuwa anajifakharisha na hatua hiyo.
-
Bunge la Somalia lapinga makubaliano ya Imarati na Somaliland
Mar 13, 2018 07:35Bunge la Federali la Somalia limepiga kura kwa kishindo kupinga makubaliano ya pande tatu kati ya eneo la Somaliland, Umoja wa Falme za Kiarabu na Ethiopia kuhusu bandari ya Berbera, iliyoko katika Ghuba ya Aden.
-
Imarati inatumia pesa zilizozuiwa za Libya kuwaunga mkono wapiganaji wa Haftar
Mar 12, 2018 13:46Makamu wa pili wa Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Libya amesema kuwa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) unatumia pesa zilizozuiwa za Libya kuwaunga mkono wapiganaji wa kamanda wa jeshi la taifa la nchi hiyo.
-
Marekani kuwekeana saini mikataba mipya ya silaha na Qatar na Imarati; Doha yaishtaki Abu Dhabi kwa UN
Mar 09, 2018 03:55Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani jana (Alkhamisi) ilisema kuwa karibuni hivi nchi hiyo itatiliana saini mikataba mipya ya silaha na Qatar na Imarati ambayo itakuwa na thamani ya dola milioni 467.
-
Ethiopia yanunua hisa za Bandari ya Berbera Somaliland
Mar 02, 2018 07:51Serikali ya Ethiopia imenunua asilimia 19 ya hisa za Bandari ya Berbera iliyoko katika Jamhuri iliyojitangazia uhuru ya Somaliland nchini Somalia.
-
Mansour Hadi avunja ukimya; aituhumu Imarati kwa kuvuruga uthabiti Yemen
Feb 13, 2018 02:57Rais wa zamani wa Yemen Abdu Rabbuh Mansour Hadi hatimaye amevunja kimya chake na kuituhumu Imarati kuwa inadhoofisha na kuvuruga hali ya uthabiti huko Yemen.
-
Mshindi wa Nobel asema Saudia na Imarati zimeisaliti Yemen
Feb 08, 2018 14:16Tawakkol Karman, mshindi wa Tuzo ya Amani ya Nobel wa nchini Yemen amesema Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu zimeisaliti nchi yake kwa kuivamia kijeshi na kuifanya ishuhudie moja ya migogoro mikubwa zaidi duniani.
-
Safari yenye malengo ya uchaguzi ya Rais wa Misri nchini Imarati
Feb 08, 2018 07:53Rais Abdul-Fatah al-Sisi wa Misri Jumanne ya juzi aliwasili Abu Dhabi katika mji mkuu wa Umoja wa Falme za Kiarabu (Imarati) baada ya kukamilisha safari yake ya siku tatu huko Oman.
-
Mkuu wa Kamati ya Masuala ya Katiba Bunge la Somalia asema: Imarati ilipanga kumuua
Feb 04, 2018 02:42Mwenyekiti wa Kamati ya Masuala ya Katiba ya Mabunge ya Somalia amesema kuwa vyombo vya ujasusi vya Imarati vilihusika na shambulizi lililolenga nyumba yake mjini Mogadishu mwishoni mwa mwezi Disemba na kwamba lengo la shambulizi hilo lilikuwa kumuua yeye.
-
Mshindi wa zawadi ya amani ya Nobel ashangaa kutoshtakiwa Bin Salman na Al Nahyan
Feb 03, 2018 08:20Bi Tawakkol Karman, mshindi wa zawadi ya amani ya Nobel wa nchini Yemen amesisitizia umuhimu wa kushtakiwa kimataifa Mohammad Bin Salman, Mrithi wa Kiti cha Ufalme nchini Saudia na Mohammed bin Zayed Al Nahyan, Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Abu Dhabi kutokana na jinai zao za mauaji ya umati nchini Yemen.