-
India na Uturuki, shabaha mpya za vita vya kiuchumi vya Trump
Mar 06, 2019 02:28Rais wa Marekani, Donald Trump anaendeleza mashambulizi na vita vyake vya kibiashara dhidi ya mataifa mengine duniani kupitia kuziongezea ushuru bidhaa za kigeni zinazoingia Marekani na hivyo kusababisha vurugu kubwa katika miamala ya kibiashara ya kimataifa.
-
Pakistan yatimua nyambizi za jeshi la India, hali ingali tete
Mar 05, 2019 10:50Pakistan inasema imeitimua kwa mafanikio nyambizi ya Jeshi la Majini la India ambayo ilijaribu kuingia katika mipaka yake ya baharini huku hali ikiwa bado ni tete baina ya madola hayo jirani yanayohasimiana na ambayo yana silaha za nyuklia.
-
OIC yazitaka India na Pakistan zitatue mgogoro kwa njia za amani
Mar 03, 2019 04:12Jumuiya ya Ushirikiano wa Nchi za Kiislamu (OIC) imepasisha azimio linalozitaka India na Pakistan zijiepushe na vitendo vinavyoweza kuendelea kuchochea taharuki baina yao, sambamba na kuupatia ufumbuzi mgogoro baina ya nchi mbili hizo jirani kwa njia za amani.
-
Pakistan yaiomba Iran ipatanishe mzozo kati yake na India
Mar 01, 2019 23:18Ubalozi wa Pakistan mjini Tehran umeiomba Jamhuri ya Kiislamu ya Kiislamu ya Iran itumie ushawishi wake kusaidia utatuzi wa amani wa mzozo uliozuka baina ya nchi yake na India.
-
Tishio la Pakistan la kuiangamiza miji ya India ya Mumbai na New Delhi
Feb 27, 2019 09:16Msemaji wa jeshi la Pakistan ametangaza kuwa, endapo kutatokea vita baina ya India na Pakistan, basi mwanzoni tu mwa vita hivyo, Pakistan itaisambaratisha miji ya Mumbai na New Delhi na kuisawazisha na udongo.
-
Katibu Mkuu wa UN ataka India, Pakistan zipunguze uhasama
Feb 20, 2019 04:31Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito kwa India na Pakistan zichukue hatua za haraka kupunguza uhasama baina yao kufuatia hujuma mbaya ya kigaidi huko Kashmir ambayo imepelekea kuwepo hatari ya kuibuka mapigano baina ya nchi hizo mbili zenye silaha za nyuklia.
-
India yaituhumu Pakistan kwa kuhusika na shambulizi la Kashmir
Feb 19, 2019 12:21Kamanda wa jeshi la India katika eneo la Kashmir Luteni Jenerali G S Dhillon amesema kuwa shirika la ujasusi la Pakistan limehusika katika hujuma iliyolenga msafara wa askari usalama wa nchi hiyo wiki iliyopita ambayo imeua zaidi ya askari 40 wa India.
-
Bahram Qassemi: Iran itatoa majibu dhidi ya vitendo vya kiuadui dhidi yake
Jan 14, 2019 23:11Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Tehran itachukua hatua ya lazima na mwafaka mkabala na kitendo chochote kile cha kiuadui ambacho kitakuwa dhidi ya maslahi ya kitaifa ya Iran.
-
Watawa wanawake wa Kanisa Katoliki nchini India wafichua ufuska wanaofanyiwa na makasisi
Jan 03, 2019 23:13Watawa wanawake wa Kanisa Katoliki nchini India wamefichua namna maaskofu, mapadri na hata makasisi wastaafu wa kanisa hilo wanavyowadhalilisha kingono wasijue cha kufanya.
-
Jitihada za India za kupunguza utegemezi kwa dola ya Marekani
Dec 15, 2018 23:16Wizara ya Biashara ya India imetangaza kuwa, nchi hiyo inafanya jitihada za kupunguza utegemezi wa nchi hiyo kwa sarafu ya dola ya Marekani.