-
Saudia yakanusha kuhusika na shambulio la Israel Hudaydah; Iran yalaani
Jul 21, 2024 03:20Wizara ya Ulinzi ya Saudi Arabia imekadhibisha ripoti za vyombo vya habari vya Israel kuwa Riyadh imeshiriki katika mashambulizi ya anga yaliyofanywa na utawala haramu wa Israel dhidi ya mji wa al-Hudaydah, magharibi mwa Yemen.
-
Blinken: Kujiondoa JCPOA ni katika makosa makubwa ya Marekani
Jul 21, 2024 03:19Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani amekiri bayana kuwa, hatua ya nchi hiyo ya kujiondoa kwenye makubaliano ya nyuklia ya JCPOA ni moja ya makosa makubwa zaidi yaliyowahi kufanywa na Washington katika miaka ya hivi karibuni.
-
Utayari wa Iran wa kushirikiana katika kuimarisha amani na usalama katika eneo
Jul 20, 2024 04:31Amir Saeid Iravani Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa, Iran iko tayari kushirikiana na nchi nyingine katika fremu ya Jumuiya ya Ushirikiano ya Shanghai na Umoja wa Mataifa ili kukabiliana na changamoto za dharura na kuimarisha amani na usalama katika eneo.
-
Iran: Pingamizi la kuundwa taifa la Palestina limeanika dhati ya ubaguzi ya Israel
Jul 19, 2024 22:50Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema hatua ya Bunge la utawala wa Kizayuni wa Israel ya kupinga kuasisiwa taifa huru la Palestina kwa mara nyingine tena imeidhihirishia dunia dhati ya ubaguzi wa rangi ya utawala huo haramu.
-
Iran: US ni kizingiti katika kupatiwa ufumbuzi masuala ya ulimwengu
Jul 19, 2024 07:39Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekosoa vikali maamuzi na hatua za mabavu na za upande mmoja zinazochukuliwa na Marekani katika masuala mbali mbali ya dunia akisisitiza kuwa, mwenendo huo unafanya hali ya mambo uliwenguni kuwa mbaya zaidi.
-
Sisitizo la viongozi wakuu wa Iran na Saudia la kuimarisha uhusiano baina ya nchi zao
Jul 19, 2024 05:26Mohammed bin Salman, mrithi wa kiti cha ufalme wa Saudi Arabia na Massoud Pezeshkian, rais mteule wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, wamezungumza kwa simu na kutilia mkazo umuhimu wa kuendeleza ushirikiano kati ya Tehran na Riyadh.
-
Iran yakosoa sera za kindumakuwili za nchi za Magharibi kuhusiana na jinai za Israel
Jul 19, 2024 00:22Katibu wa Baraza la Haki za Binadamu la Iran amekosoa madai yaliyotolewa dhidi ya Ripota Maalumu wa Umoja wa Mataifa katika Masuala ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu na misimamo ya kindumakuwili kuhusiana na maripota maalumu wa jumuiya hiyo ya kimataifa.
-
Kanusho la Iran kwa madai ya uwongo ya Marekani ya kuhusika katika jaribio la kumuua Trump
Jul 18, 2024 07:10Baada ya tukio la kupigwa risasi Donald Trump, rais wa zamani na mgombea wa chama cha Republican katika uchaguzi wa rais wa Marekani wa 2024, baadhi ya vyombo vya habari vya Marekani kwa mara nyingine vikiendeleza propaganda za chuki dhidi ya Iran (Iranphobia) vilidai kuweko mkono wa Iran katika tukio hilo.
-
Mrithi wa Ufalme wa Saudia ampongeza Rais mteule wa Iran
Jul 17, 2024 10:16Mrithi wa Kiti cha Ufalme wa Saudi Arabia, Mohammad Bin Salman amemnyooshea mkono wa pongezi Masoud Pezeshkian, Rais Mteule wa Iran kwa kuibuka mshindi katika duru ya pili ya uchaguzi wa 14 wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Bagheri Kani na Rais wa Baraza Kuu la UN wajadili mauaji ya Gaza
Jul 16, 2024 04:14Kaimu Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuna udharura wa kuchukuliwa hatua za kivitendo ili kukomesha jinai zinazofanywa na utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Wapalestina wa Ukanda wa Gaza.