-
Mufti Mkuu wa Russia: Umma wa Kiislamu unapaswa kusimama pamoja na Iran dhidi ya njama za shetani
May 02, 2026 07:35Mufti Mkuu na Mkuu wa Idara ya Masuala ya Kidini ya Waislamu wa Russia ameeleza kuwa, Umma wa Kiislamu unapaswa kusimama pamoja na Iran dhidi ya njama za Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel na akasema: "Iwapo Waislamu watakuwa na umoja na mshikamano, kambi ya shetani haiwezi kamwe kurudia uchokozi dhidi ya Gaza, Syria, Iran na Lebanon."
-
Mbunge wa Kongresi: Ni mwehu anayedai Marekani imeshinda vita dhidi ya Iran
May 02, 2026 07:25Mwakilishi wa cha cha Democratic wa California katika Kongresi ya Marekani, Sara Jacobs, amemkosoa vikali Waziri wa Vita wa nchi hiyo, Pete Hegseth kwa kutangaza ushindi dhidi ya Iran, akitaja madai hayo kuwa ni udanganyifu.
-
Mipaka yetu ni mirefu kuliko kuta mbili kote Marekani: Spika Qalibaf akejeli mzingiro wa Marekani
May 02, 2026 07:23Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Baqer Qalibaf amekejeli mzingiro wa jeshi la majini la Marekani dhidi ya Iran, akieleza kuwa mipaka mirefu ya nchi hiyo inabatilisha jaribio lolote la kuizingira Jamhuri ya Kiislamu.
-
IRGC: Manowari za Marekani zitateketea ikiwa Iran itashambuliwa tena
May 01, 2026 08:13Kamanda wa Kikosi cha Anga cha Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Brigedia Jenerali Seyyed Majid Mousavi, amesema Iran itajibu uchokozi wowote wa adui kwa mashambulizi ya muda mrefu na yenye kuumiza, akibainisha kuwa meli za kivita za Marekani zitapata hatima sawa na vituo vya kijeshi vya Marekani katika eneo la Asia Magharibi.
-
Rais wa Iran: Mzingiro wa kijeshi baharini ni tishio kwa amani ya dunia
May 01, 2026 08:04Rais wa Iran: Mzingiro wa kijeshi baharini ni tishio kwa amani ya dunia
-
Kiongozi Muadhamu: Iran itaweka “kanuni mpya za kisheria” katika Mlango wa Bahari wa Hormuz
Apr 30, 2026 13:59Ayatullah Seyyed Mojtaba Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, ametangaza mwanzo wa “sura mpya” kwa Mlango Bahari wa Hormuz, njia ya kimkakati ya baharini.
-
Mkuu wa Jeshi la Wanamaji la Iran: Wamarekani wanaogopa silaha yetu mpya
Apr 30, 2026 10:57Kamanda wa Jeshi la Wanamaji la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, amesema kwamba majeshi ya Iran yameufunga Mlango Bahari wa Hormuz kutoka Bahari ya Arabia, akisisitiza kwamba: Adui atakutana na silaha yetu ambayo anaiogopa sana.
-
Qalibaf ajibu madai ya Trump na Waziri wa Fedha wa US
Apr 30, 2026 10:21Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran (Bunge) amejibu madai ya Rais wa Marekani na majigambo ya Waziri wa Fedha wa utawala huo wa kigaidi kupitia ujumbe uliotumwa katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa X.
-
Iran yaitaka ICRC kufuatilia kisheria ukiukwaji wa haki za binadamu katika vita vya siku 40
Apr 30, 2026 08:12Mkuu wa Jumuiya ya Hilali Nyekundu ya Iran (IRCS), katika kikao na Rais wa Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC), ameitaka taasisi hiyo ya kimataifa kuiunga mkono Jumuiya ya Hilali Nyekundu na wananchi wa Iran katika kufuatilia kisheria ukiukwaji wa haki za kibinadamu uliofanyika katika vita vya siku 40 vya Marekani na Israel dhidi ya nchi hii.
-
Afisa wa Hizbullah: Mapambano yataendelea hadi ukombozi kamili wa ardhi ya Lebanon
Apr 30, 2026 07:42Makamu wa Mwenyekiti wa Baraza la Kisiasa la harakati ya Hizbullah ya Lebanon amesisitiza msimamo wa msingi wa harakati hiyo kuhusu uvamizi wa utawala wa Kizayuni wa Israel na kusema kuwa Muqawama na mapambano yataendelea hadi ardhi yote ya nchi hiyo itakapokombolewa kikamilifu.