-
Iran na Zimbabwe zatathmini njia za kuimarisha uhusiano wao
Nov 06, 2022 04:18Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Zimbabwe hapa mjini Tehran, na kujadili mikakati na njia za kupanua na kuboresha uhusiano wa pande mbili wa nchi hizi mbili.
-
Jibu la Rais wa Iran kwa bwabwaja na njozi za Biden
Nov 05, 2022 07:57Rais Sayyid Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika marasimu ya kukumbuka tarehe 13 Aban ambayo inaadhimishwa hapa nchini kama Siku ya Kitaifa ya Kupambana na Uistikbari Duniani kwamba: Marekani ina nafasi ya kwanza katika vita na umwagaji damu na inaangamiza na kuharibu maslahi ya mataifa mengine ili kujidhaminia maslahi yake. Rais wa Iran ameeleza hayo katika radiamali yake kwa matamshi ya Joe Biden ya kuuunga mkono ghasia na fujo nchini Iran.
-
Sheikh Kazem Sediqi: Lengo la Marekani ni kuchochea hisia za kikaumu nchini Iran
Nov 04, 2022 08:24Khatibu wa Swala ya Ijumaa iliyoswaliwa leo hapa mjini Tehran amesema kuwa, lengo la utawala wa Marekani katika fitina na vurugu za hivi karibuni hapa Iran ni kuchochea hisia za kikaumu na kuzusha vita vya ndani katika taifa hili.
-
Imam wa msikiti auawa katika shambulio la kigaidi mkoani Sistan na Baluchistan kusini mwa Iran
Nov 04, 2022 03:15Mkuu wa Polisi wa Sistan na Baluchistan ya Iran amesema: Kabla ya Sala ya Magharibi hapo jana Imamu wa msikiti wa Moulay-e-Mottaqian katika mji wa Zahedan, kusini mashariki mwa Iran, aliuawa shahidi kwa kupigwa risasi na magaidi.
-
China, Russia zapinga mkutano usio rasmi wa Baraza la Usalama la UN dhidi ya Iran
Nov 03, 2022 22:52China na Russia zimelaani kuitishwa mkutano wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran. Wawakilishi wa China na Russia wamelaani kitendo cha Marekani na Albania cha kufanya mkutano usio rasmi wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu eti matukio ya Iran.
-
Iran yatangaza vikwazo dhidi ya shakhsia na taasisi ya Canada
Nov 03, 2022 08:19Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetangaza kuwa imeyaweka majina ya shakhsia na taasisi ya Canada kwenye orodha yake ya vikwazo, kwa kuunga mkono ugaidi.
-
Umoja wa Mataifa waionya Twitter kuhusu matamshi ya kueneza chuki, ubaguzi
Nov 01, 2022 23:17Rekodi mbaya ya mmiliki mpya wa Twitter, Elon Musk ya kuchukua misimamo isiyo ya kawaida na kuibua masuala yenye utata imeufanya Umoja wa Mataifa kumuonya dhidi ya kuchapisha maudhui yoyote ya chuki katika mtandao wa kijamii wa Twitter.
-
Kataib Hizbullah ya Iraq: Riyadh imeanzisha mashine chafu ya propaganda dhidi ya Iran
Oct 27, 2022 23:24Harakati ya Kataib Hizbullah ya Iraq imetangaza kwamba Saudi Arabia inaendeleza harakati yake chafu na ya kichochezi dhidi ya Iran na inatumia vyombo vyake vya habari na makundi ya kitakfiri na kigaidi katika mwelekeo huo.
-
Raisi: Shambulio la kigaidi dhidi ya Haram Tukufu mjini Shiraz halitapita bila jibu
Oct 27, 2022 04:46Rais wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu itatoa jibu kali na la kujutisha kwa wale waliohusika katika shambulio la kigaidi dhidi ya Haram Tukufu ya Shah Cheragh mjini Shiraz, kusini magharibi mwa nchi.
-
Dunia yalaani shambulio la umwagaji damu nchini Iran
Oct 27, 2022 04:44Jamii ya kimataifa imeendelea kutuma salamu za rambirambi na kutoa taarifa za kulaani shambulio la kigaidi lililopelekea kuuawa na kujeruhiwa makumi ya watu kusini magharibi mwa Iran.