-
Raisi: Iran na Turkmenistan zina uhusiano uliokita mizizi
Jun 15, 2022 07:55Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema uhusiano wa pande mbili wa nchi hii na Turkmenistan ni wa kidugu na uliokita mizizi.
-
Kauli zisizo za kirafiki za Fuad Hussein; ulazima wa kutoa ufafanuzi uko kwa Iran au Iraq?
Jun 15, 2022 03:39Waziri wa mambo ya nje wa Iraq, kwa mara ya kwanza ametoa matamshi ya kuituhumu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwamba inaingilia masuala ya ndani ya nchi yake na kudai kuwa uhusiano wa Iran na Iraq umetoka kwenye hatua ya "ukimya" na kufikia hatua ya kuhitajika "ufafanuzi".
-
Wabunge wa Iran: IAEA imepoteza itibari ya kiufundi
Jun 13, 2022 06:28Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) imesema hatua ya Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki (IAEA) ya kupasisha azimio dhidi ya Iran imeonesha wazi kuwa taasisi hiyo ya Umoja wa Mataifa imepoteza itibari yake ya kiufundi.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu kuwa mapambano ndio njia pekee ya kufikia ushindi dhidi ya Marekani
Jun 12, 2022 04:33Akizungumza jana Jumamosi alasiri katika kikao na Rais Nicolas Maduro wa Venezuela na ujumbe alioandamana nao, Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesisitiza juu ya kusimama imara Iran na Venezuela mbele ya mashinikizo makali na vita vya pande kadhaa vya Marekani na kusisitiza: Uzoefu wa mafanikio wa nchi mbili unaonyesha kwamba njia pekee ya kukabiliana na mashinikizo hayo ni mapambano na kusimamam imara.
-
Kundi la kwanza la mahujaji wa Kiirani laondoka nchini kwenda Saudia
Jun 12, 2022 03:27Kundi la kwanza la wananchi wa Iran wanaokwenda kutekeleza ibada tukufu ya Hija limeondoka nchini mapema leo Jumapili kwenda katika mji mtukufu wa Madina nchini Saudi Arabia.
-
Abdollahian: Azimio la IAEA dhidi ya Iran lilichochewa kisiasa
Jun 12, 2022 03:26Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amezikosoa vikali Marekani na nchi tatu za Ulaya za Uingereza, Ufaransa na Ujerumani, kwa kuwasilisha azimio dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu mbele ya Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA.
-
Abdollahian: Iran haina vizingiti katika kukuza ushirikiano wake na Nigeria
Jun 12, 2022 00:14Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Tehran haina vizingiti vyovyote katika njia ya kustawisha uhusiano wake na Nigeria.
-
Kiongozi Muadhamu: Muqawama ndio njia pekee ya kuzima mashinikizo ya Marekani
Jun 11, 2022 22:57Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema uzoefu wenye mafanikio wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Venezuela katika kupambana na vikwazo vya Marekani umedhihirisha wazi kuwa, muqawama ndio njia pekee ya kuzima mashinikizo ya namna hiyo.
-
Iran yakosoa shambulio la Israel dhidi ya Damascus, mji mkuu wa Syria
Jun 11, 2022 05:48Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amelaani hatua ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kufanya shambulio dhidi ya Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Damascus, mji mkuu wa Syria na kusisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itaendelea kuliunga mkono taifa hilo la Kiarabu.
-
Rais Maduro wa Venezuela aitembelea Iran kwa ziara ya siku 2
Jun 10, 2022 22:10Rais Nicolas Maduro wa Venezuela aliwasili hapa Tehran jana Ijumaa kwa safari rasmi ya kikazi ya siku mbili ya kuitembelea Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.