-
Rais Maduro wa Venezuela aitembelea Iran kwa ziara ya siku 2
Jun 10, 2022 22:10Rais Nicolas Maduro wa Venezuela aliwasili hapa Tehran jana Ijumaa kwa safari rasmi ya kikazi ya siku mbili ya kuitembelea Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Russia: Azimio la IAEA dhidi ya Iran ni la kipumbavu
Jun 10, 2022 21:58Mwakilishi wa Kudumu wa Russia katika taasisi za kimataifa zenye makao yao mjini Vienna, Austria amelitaja azimio lililopasishwa hivi karibuni na Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA dhidi ya Iran kuwa ni la kipumbavu.
-
Iran na Venezuela zasaini makubaliano ya ushirikiano ya miaka 20
Jun 11, 2022 06:46Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na mwenzake wa Venezuela, Nicolas Maduro wamesaini makubaliano ya kuimarisha ushirikiano ya miaka 20, yenye lengo la kupiga jeki uhusiano wa nchi mbili hizi katika nyuga mbalimbali.
-
Iran: Tutatoa jibu madhubuti kwa azimio la US, EU lililopasishwa na IAEA dhidi yetu
Jun 09, 2022 18:52Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani kitendo cha Bodi ya Magavana ya Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA cha kupasisha azimio dhidi ya Tehran na kusisitiza kuwa, taifa hili litatoa jibu mwafaka na madhubuti kwa hatua hiyo.
-
Msimamo hafifu na dhaifu wa Mkuu wa IAEA kuhusu hujuma zilizofanywa kwenye vituo vya nyuklia vya Iran
Jun 08, 2022 07:18Rafael Grossi, Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA jana Jumanne alifanyiwa mahojiano makao makuu ya wakala huo mjini Vienna; na moja ya masuali aliyoulizwa ni kuhusu takwa la Iran la kumtaka alaani hujuma zilizofanywa dhidi ya vituo vyake vya nyuklia.
-
Jenerali: Tutateketeza Tel Aviv, Haifa iwapo Israel itafanya kosa dhidi ya Iran
Jun 08, 2022 06:19Kamanda wa vikosi vya nchi kavu vya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ameonya kuwa, Tehran itaiteketeza miji ya Tel Aviv na Haifa iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utajaribu kufanya kosa lolote dhidi ya taifa hili.
-
Iran yasikitishwa na shambulio la kigaidi lililoua makumi Nigeria
Jun 07, 2022 03:39Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani shambulio la kigaidi lililoua makumi ya watu kanisani huko Nigeria hivi karibuni, sanjari na kutoa mkono wa pole kwa serikali ya Abuja na familia za raia wa nchi hiyo ambao waliuawa katika hujuma hiyo.
-
Abdollahian: Iran itaendelea kuunga mkono muqawama wa Palestina
Jun 06, 2022 23:03Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu katu haitoruhusu kukanyagwa haki za Wairani katika mazungumzo (ya Vienna) au kupuuza haki za wananchi Waislamu wa Palestina na kueleza bayana kuwa, Tehran itaendelea kuunga mkono muqawama wa Wapalestina.
-
Sisitizo la Waziri wa Uchumi na Fedha wa Iran kuhusu kushirikiana nchi za Kiislamu kwa ajili ya kuimarisha uchumi.
Jun 06, 2022 05:38Akizungumza Jumamosi katika kikao cha kila mwaka cha Baraza Kuu la Benki ya Maendeleo ya Kiislamu IDB huKo mjini Cairo Misri, Ehsan Khandouzi, Waziri wa Masuala ya Kiuchumi na Fedha wa Iran, amesisitiza juu ya ulazima wa nchi za Kiislamu kushirikiana kwa ajili ya kuimarisha uthabiti wa kiuchumi wa nchi hizo na kuufanya kuwa na misingi madhubuti zaidi katika kukabiliana na changamoto zilizopo na za baadaye.
-
Iran yamuita balozi wa India kulalamikia kauli za kumvunjia heshima Mtume Muhammad SAW
Jun 05, 2022 23:06Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imemuita balozi wa India mjini Tehran kulalamikia vikali matamshi dhidi ya Mtume Mutukufu wa Uislamu, Muhammad SAW ambayo yalitolewa katika mdahalo wa televisheni huko India na kuibua hasira miongoni mwa Waislamu duniani.