-
Corona na jitihada za madaktari walioko mstari wa mbele wa kupambana na virusi visivyojali mipaka
Feb 28, 2020 08:55Wimbi la kuenea virusi hatari vya corona duniani sasa hivi limekuwa ndiyo daghadagha na wasiwasi mkubwa wa nchi zote huku jamii ya madaktari nchini Iran ikiwa mstari wa mbele kwa kufanya kazi usiku na mchana katika kupambana na virusi hivyo vinavyoenea kwa kasi.
-
Waziri wa Afya: Mapambano ya Iran dhidi ya virusi vya Corona yatawashangaza walimwengu
Feb 28, 2020 08:30Waziri wa Afya wa Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu itaushangaza ulimwengu kutokana na mbinu yake ya kupambana na maambukizi ya virusi vya Corona.
-
Hatua ya kukurupuka ya Marekani ya kumuwekea vikwazo Katibu Mkuu wa Kataeb Hizbullah ya Iraq
Feb 28, 2020 02:05Marekani imetuma idadi kubwa ya wanajeshi wake huko Iraq tangu mwaka 2014 kwa kisingizio cha kupambana na kundi la Daesh. Katika hatua yake ya kukurupuka Marekani imeliorodhesha jina la kiongozi wa mojawapo ya makundi muhimu ya taasisi ya Kataeb Hizbullah ya Iraq licha ya nafasi muhimu ya kundi la kujitolea la wananchi la al Hashd al Shaabi katika kutoa pigo na kuliangamiza kundi la kigaidi la Daesh huko Iraq.
-
Hemmati: Iran ina uhusiano wa kimataifa wa kibenki usioweza kuwekewa vikwazo
Feb 27, 2020 09:37Gavana wa Benki Kuu ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu imebuni uhusiano wa kibenki wa kimataifa usioweza kuwekewa vikwazo na wala usiohusiana na jopokazi la eti kupambana na utakatishaji wa fedha chafu linalojulikana kwa kimombo kama Financial Action Task Force (FATF).
-
Russia: tutapinga kurejeshwa vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi ya Iran
Feb 26, 2020 23:24Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Russia amevitaja vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran kuwa kinyume cha sheria na kueleza kuwa Moscow itapinga juhudi zozote kwa lengo la kuirejeshea Tehran vikwazo vya Umoja wa Mataifa.
-
Naibu Waziri wa Afya wa Iran apatwa na Corona, asema nchi itashinda virusi hivyo wiki chache zijazo
Feb 25, 2020 12:18Naibu Waziri wa Afya wa Iran amethibitisha kuwa amepatwa na virusi vya Corona lakini amesisitiza kuwa, nchi hii itashinda janga la virusi hivyo wiki chache zijazo.
-
Nchi zilizoliwekea taifa la Iran vikwazo vya madawa ni katili
Feb 25, 2020 04:26Mkuu wa Baraza la Haki za Binadamu la Idara ya Mahakama ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema nchi ambazo zinazuia madawa kuingia hapa nchini ni katili na wauaji wa binadamu.
-
Hatua ya kisiasa ya FATF ya kuiweka Iran katika orodha nyeusi
Feb 22, 2020 08:01Nchi za Magharibi huku zikiongozwa na Marekani kwa muda sasa zimekuwa zikizingatia na kutilia maanani utekelezaji wa siasa za mashinikizo ya pande zote kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran lengo likiwa ni kujaribu kubadilisha misingi na siasa za nchi hii.
-
Ujerumani yaitaka Saudi Arabia ichunge haki za binadamu
Feb 22, 2020 03:50Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani amewataka viongozi wa Saudi Arabia wafanyie marekebisho sheria zao na wachunge haki za binadamu.
-
Mousavi: Wairani hawaithamini Marekani wala vikwazo vyake dhidi yao
Feb 21, 2020 23:14Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa radimali yake kufuatia hatua ya Marekani ya kuwawekea vikwazo wanachama wa Baraza la Wanazuoni Wataalamu wanaomchagua Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu na kusema kuwa, serikali, taifa na nguzo zote za Jamhuri ya Kiislamu haziipi thamani Marekani wala vikwazo vyake vya kidhalimu.