-
Washington yalazimika kuzingatia msamaha kwa wanunuzi wa mafuta ya Iran
Oct 22, 2018 04:45Waziri wa Fedha wa Marekani amelegeza msimamo wa nchi hiyo katika kuyawekea kikamilifu vikwazo mafuta ya Iran na kutangaza kuwa Washington inafikiria suala la msamaha kwa wanunuzi wa mafuta ya Iran.
-
Syria yasisitiza kuwa itaendelea kuimarisha uhusiano wake wa kiuchumi na Iran
Oct 20, 2018 12:20Katibu Mkuu wa Umoja wa Wafanyabiashara wa Syria amesema kuwa, kuna haja ya kuondolewa vizuizi vyote hata vidogo vidogo katika juhudi za kuimarisha uhusiano wa pande zote wa kiuchumi baina ya nchi mbili ndugu za Iran na Syria.
-
Nchi za Ulaya na Asia zataka kuondolewa vikwazo Iran
Oct 20, 2018 04:34Nchi za Ulaya na Asia sanjari na kutangaza utayarifu wao wa kuendelea kufungamana na makubaliano ya nyuklia ya Iran, zimesema kuondolewa vikwazo Jamhuri ya Kiislamu ni sehemu muhimu ya mapatano hayo ya kimataifa yanayofahamika kama JCPOA.
-
Iran, Uturuki, Russia na India zaitisha kikao Ankara kuipiga teke sarafu ya dola ya Marekani
Oct 19, 2018 21:39Kikao cha "Changamoto na Fursa za Biashara kwa Fedha za Taifa" kilifanyika jana Ijumaa mjini Ankara Uturuki na kushirikisha maafisa na wataalamu kutoka nchi za Iran, Uturuki, Russia na India.
-
Facebook: Iran na Korea Kaskazini hazijahusika kuiba taarifa za watumiaji wa mtandao wetu
Oct 19, 2018 11:35Shirika la Mtandao wa Kijamii la Facebook limekadhibisha tuhuma kwamba Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Korea Kaskazini zimehusika kudukua taarifa za watumiaji wa mtandao huo.
-
Zarif: Vikwazo vipya vya US dhidi ya Iran vinakiuka maamuzi ya ICJ
Oct 18, 2018 10:34Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema Marekani imekubuhu na ni mraibu mkubwa wa kuyawekea mataifa mengine vikwazo, na kwamba vikwazo vipya dhidi ya Tehran ni ukiukaji wa moja kwa moja kwa maamuzi ya hivi karibuni ya Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu (ICJ).
-
Misimamo na hatua za upande mmoja za Trump; hatari kwa jamii ya kimataifa
Oct 18, 2018 05:51Mwakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesema kuwa jamii ya kimataifa inapasa kwa uchache kukabiliana na hatua za Marekani za kukiuka na kuvunja sheria ili kulinda heshima yake.
-
Waziri wa Mafuta wa Iran: Marekani lazima iondoe vikwazo ili bei ya mafuta ishuke
Oct 17, 2018 00:48Bijan Namdar Zangeneh, Waziri wa Mafuta wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, iwapo Marekani itaiondolea vikwazo Iran, bei ya mafuta katika soko la dunia itapungua na hali ya kuvurugika uthabiti iliyopo katika soko hilo hivi sasa itaondoka.
-
Qassemi: Iran na Afghanistan zina historia kongwe katika uhusiano wa pande mbili
Oct 15, 2018 10:42Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Afghanistan ni jirani muhimu wa Iran na kwamba, historia kongwe iliyoko katika uhusiano wa pande mbili inalazimu nchi hizo kuwa na ushirikiano zaidi katika nyuga mbalimbali.
-
Waziri wa Ulinzi wa Iran aonya kuhusu kuibuka 'Hitler' wapya
Oct 15, 2018 10:11Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametahadharisha kuwa, iwapo dunia itaendelea kufumbia macho ukiukwaji wa sheria za kimataifa unaofanywa na baadhi ya madola ya kibeberu, basi ijiandae kushuhudia watawala madikteta na makatili kama Adolf Hitler, kiongozi wa zamani wa Kinazi nchini Ujerumani.