-
Iran yalaani mashambulizi ya karibuni ya Israel kusini mwa Lebanon
Oct 18, 2025 04:19Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani mashambulizi ya karibuni ya anga ya Israel kusini mwa Lebanon, na kuzibebesha dhima nchi zilizodhamini makubaliano ya kusitisha vita yaani Ufaransa na Marekani kwa kutoichukulia hatua Israel.
-
Yazdanian: Iran hurusha satelaiti sita angani kila mwaka
Oct 18, 2025 04:18Vahid Yazdanian Mkurugenzi wa Kituo cha Utafiti wa Anga cha Iran ametangaza kuwa Iran imefanikiwa kurusha satelaiti sita angani kila mwaka, sambamba na kupiga hatua kubwa katika teknolojia ya kurusha satelaiti.
-
Unyanyuaji Uzani; Muirani avunja rekodi ya dunia, ashinda dhahabu Misri
Oct 17, 2025 03:20Ali Akbar Gharibshahi, bingwa wa mchezo wa kunyanyua vitu vizito wa Iran ameweka rekodi mpya ya dunia na kushinda medali ya dhahabu katika kategoria ya kilo wanamichezo wenye 107, kwenye Mashindano ya Dunia ya Kunyanyua Uzani ya 2025 nchini Misri.
-
Pezeshkian: Vijana wa Iran wamebobea katika uzalishaji wa makombora
Oct 16, 2025 23:12Rais Masoud Pezeshkian wa Iran ameashiria uwezo wa kustaajabisha wa vijana wa Jamhuri ya Kiislamu na kusisitiza kuwa, vijana wa taifa hili ndio ambao wanatengeneza makombora na nishati ya nyuklia kwa kutegemea uwezo wao.
-
Kharrazi: Iran iko tayari kwa mazungumzo, lakini haitakubali kuburuzwa
Oct 16, 2025 06:12Mkuu wa Baraza la Kistratijia la Mahusiano ya Kigeni ya Iran, Kamal Kharrazi amesema Jamhuri ya Kiislamu iko tayari kwa mazungumzo, lakini katu haitakubali kutwishwa matakwa ya aina yoyote.
-
Waziri: Mamilioni ya watalii wameitebelea Iran ndani ya miezi 6
Oct 16, 2025 02:08Zaidi ya watalii milioni 3.5 wa kigeni wameitembelea Iran katika miezi sita ya kwanza ya mwaka huu, Waziri wa Turathi za Utamaduni, Utalii na Sanaa, Reza Salehi Amiri alisema hayo jana Jumatano.
-
Mauzo ya chuma ya Iran nje ya nchi yaongezeka kwa 26%
Oct 15, 2025 08:21Thamani ya mauzo ya madini ya chuma ya Iran ilipanda hadi karibu dola bilioni 4 katika nusu ya kwanza ya mwaka huu 2025, na kuashiria ongezeko la asilimia 26 ya mauzo hayo kwa mwaka.
-
Iran: Trump hawezi kuwa mtu wa kuleta amani wakati anachochea vita visivyo na mwisho
Oct 15, 2025 02:33Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Abbas Araghchi amemkosoa vikali Donald Trump kwa sera yake ya kuchochea vita katika eneo la Asia Magharibi, akisema rais wa Marekani hawezi kudai anapigania kuleta amani katika eneo hili huku akifuata sera za uchokozi na kufungamana na "wahalifu wa kivita."
-
Araghchi kuhudhuria mkutano wa NAM nchini Uganda
Oct 14, 2025 23:04Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu, Abbas Araghchi atazuru Uganda karibuni hivi kushiriki Mkutano wa 19 wa Mawaziri wa Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote (NAM).
-
Iran: Dunia iwe macho, isikubali Israel ikiuke usitishaji vita Gaza
Oct 13, 2025 08:47Iran imesisitiza uungaji mkono wake usioyumba kwa juhudi zozote zinazolenga kukomesha mauaji na mauaji ya halaiki ya Israel huko Gaza, ikionya kuhusu historia ya utawala unaoikalia kwa mabavu Quds ya kukanyaga mikataba na makubaliano.