-
Iran yalaani vikali shambulio la Israel kusini mwa Lebanon lililoua watu na kusababisha hasara kubwa
Oct 12, 2025 02:55Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani vikali mashambulio ya kijeshi yanayofanywa kila mara na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Lebanon na kuendelea kukiuka mamlaka ya utawala na umoja wa ardhi ya nchi hiyo hususan shambulio la jana Jumamosi la ndege zisizo na rubani lililolenga kijiji cha Al-Musayleh.
-
"Israel haiaminiki; Iran inaunga mkono kusimamishwa mauaji ya kimbari Gaza"
Oct 11, 2025 23:29Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Abbas Araghchi amesema Jamhuri ya Kiislamu inakaribisha kusitishwa kwa mauaji ya kimbari ya utawala wa Israel katika Ukanda wa Gaza, huku akitoa indhari juu ya tabia ya kutokuwa na muamana Tel Aviv kwa kukiuka makubaliano kadhaa ya huko nyuma.
-
Wananchi wa Iran waandamana; waitaka Israel iheshimu kikamilifu makubaliano ya kusitisha vita Gaza
Oct 10, 2025 23:07Umati mkubwa wa wakazi wa mji wa Tehran na miji mingine kote Iran jana waliandamana kwa lengo la kuiunga mkono Palestina na kuonyesha mshikamano kwa wakazi wa Ukanda wa Gaza.
-
Iran: Maadui wanajua watalazimika ‘kuomba usitishaji vita’ iwapo watatushambulia tena
Oct 10, 2025 03:29Makamu wa Rais wa Iran, Mohammad Reza Aref amesema matukio ya hivi karibuni yameonyesha nguvu ya Jamhuri ya Kiislamu na kutangaza kwamba, maadui sasa wanatambua shambulio lolote dhidi ya taifa hili litawalazimu "kuomba kusitishwa kwa mapigano."
-
Putin: Israel imeniomba niipe Iran ujumbe kwamba haitaki vita
Oct 10, 2025 02:44Rais wa Russia, Vladmir Putin amesema viongozi wa Israel wamemtaka aieleze Iran kwamba, utawala huo haufuatilii vita na makabiliano zaidi na Iran, na una hamu ya kupunguza mvutano.
-
Iran: Tunaunga mkono mpango wowote wa kumaliza vita, mauaji ya kimbari Gaza
Oct 09, 2025 23:51Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imesisitiza kwa mara nyingine tena kwamba Jamhuri ya Kiislamu daima inaunga mkono mpango wowote unaolenga kukomesha vita na mauaji ya halaiki huko Gaza, na kusisitiza ulazima wa kuwa macho mkabala wa hulka ya utawala wa Israel ya kukiuka ahadi na makubaliano.
-
Pezeshkian: Iran ipo tayari kuimarisha uhusiano na Ivory Coast
Oct 08, 2025 09:15Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu imejiandaa kikamilifu kupanua ushirikiano wa pande mbili na Ivory Coast ili kufikia malengo ya pamoja.
-
Jeshi la majini la Iran lasaini hati ya ushirikiano wa kimkakati na nchi za eneo la Kaspi zenye ukanda wa pwani
Oct 08, 2025 08:59Makamanda wa majeshi ya majini ya Iran, Russia, Kazakhstan na Azerbaijan wametia saini mkataba wa ushirikiano wa kimkakati unaolenga kuimarisha usalama katika maji ya pamoja.
-
Araghchi: Israel inatumia mamilioni ya dola kulipa watu waongope mitandaoni
Oct 07, 2025 03:50Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran, Sayyid Abbas Araghchi ameshutumu kampeni ya propaganda iliyofichuliwa hivi karibuni ya Israel, yenye lengo la kuhamasisha uungwaji mkono kwa utawala huo kwenye mitandao ya kijamii.
-
Iran yaibuka ya 3 katika Mashindano ya Riadha ya Walemavu India
Oct 07, 2025 02:38Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imemaliza katika nafasi ya tatu katika Duru ya 12 ya Mashindano ya Riadha ya Walemavu yaliyofanyika nchini India.