-
Jibu la Iran kwa ombi la Kundi la G7 kwa ajili ya kufanya mazungumzo
Jul 02, 2025 02:21Mawaziri wa Mambo ya Nje wa kundi la nchi saba tajiri kwa viwanda G7 wametoa wito wa "kuanzishwa tena mazungumzo ya nyuklia" na Iran na kufikiwa makubaliano "jumuishi na ya kudumu" kuhusu mpango wake wa nyuklia.
-
UN: Israel imekiuka sheria za kimataifa kwa kuwalenga raia wa Iran
Jul 01, 2025 23:14Ofisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa imetangaza kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel umekiuka pakubwa sheria za kimataifa kwa kuwaua shahidi wanafamilia wa wanasayansi wa nyuklia na raia wa kawaida wa Iran.
-
Meja Jenerali Safavi azionya Marekani na Israel: Ulipizaji kisasi ujao utakuwa wa nguvu zaidi
Jul 01, 2025 08:59Mshauri wa ngazi ya juu wa masuala ya kijeshi wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amewaonya wapinzani kwamba amewaonya wapinzani kwamba duru ijayo ya mashambulizi ya kulipiza kisasi ya Iran, endapo kutafanyika uchokozi mpya dhidi ya Iran, itakuwa ya nguvu zaidi kuliko wakati wa vita vya siku 12 vya Israel dhidi ya nchi hii.
-
Iran yalitaka Baraza la Usalama la UN kuzitambua Israel na Marekani kama pande zilizoanzisha uchokozi
Jun 30, 2025 04:16Abbas Araqchi Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa liutambue utawala wa Israel na Marekani kuwa pande zilizoanzisha vita vya karibuni vya siku 12 dhidi ya Jamburi ya Kiislamu ya Iran.
-
Baqaei: Iran inataka amani lakini haitasalimu amri mbele ya ukandamizaji
Jun 28, 2025 07:44Esmaile Baqaei Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa Iran imejidhatiti kwa ajili ya suala la amani, lakini kwamba haitasalimu amri abadan mbele ya maadui
-
Pezeshkian: Vita vingeenea Mgharibi mwa Asia kama uchokozi wa Wazayuni usingejibiwa
Jun 28, 2025 04:23Rais Masoud Pezeshkian wa Iran amesema kuwa vita vya pande zote vingeshuhudiwa katika eneo zima la Magharibi mwa Asia iwapo hujuma ya uchokozi wa Israel ingesalia bila ya jibu.
-
Araghchi: Msamiati wa ‘Kusalimu Amri’ haumo kwenye fasihi ya watu wa Iran
Jun 28, 2025 03:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Abbas Araghchi amesema, kama alivyobainisha Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi, hakuna msamiati wa kusalimu amri katika fasihi ya kisiasa na fasihi ya wananchi wa Iran na kwamba wananchi hao wamethibitisha na kulionyesha vizuri hilo katika kipindi cha siku 12.
-
Seneta wa Marekani: Mpango wa nyuklia wa Iran haujaangamizwa
Jun 28, 2025 02:56Chris Murphy, Seneta wa Marekani wa chama cha Democratic amesema, madai ya rais wa nchi hiyo Donald Trump kuhusu kuangamizwa mpango wa nyuklia wa Iran hayana ukweli.
-
Balozi wa Iran UN: Israel itawajibishwa kwa mauaji ya makusudi ya watoto Wairan
Jun 28, 2025 02:53Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa Amir Saeid Iravani amelaani sera ya utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuua watoto makusudi katika inavyoanzisha katika kanda ya Asia Magharibi na kusisitiza kuwa utawala huo haramu utawajibishwa kwa jinai zake hizo za kuua watoto wadogo.
-
Katibu Mkuu wa Hizbullah: Iran ndiye mshindi wa Vita vya Siku 12
Jun 28, 2025 02:49Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon amesema, Iran ndiye mshindi wa makabiliano baina yake na adui mzayuni.