-
UN: DAESH (ISIS) imeacha makaburi ya halaiki zaidi ya 200 yenye maelfu ya viwiliwili nchini Iraq
Nov 06, 2018 12:58Makaburi zaidi ya 200 ya halaiki ambayo ndani yake yana maelfu ya viwiliwili yamegunduliwa katika maeneo kadhaa nchini Iraq yaliyokuwa yakikaliwa na kundi la kigaidi na ukufurishaji la DAESH (ISIS).
-
Rais Rouhani: Marekani itafeli tu katika njama zake mpya dhidi ya Iran
Oct 31, 2018 12:22Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, licha ya kuwepo vikwazo vya Marekani dhidi ya Tehran, lakini nchi nyingi duniani za Asia na Ulaya zina hamu ya kuendeleza ushirikiano wao na Iran.
-
Wafanyaziara milioni 15 wamefika Karbala kushiriki kwenye Arubaini ya Imam Hussein (as)
Oct 30, 2018 03:56Baraza la Mkoa wa Karbala nchini Iraq limetangza kuwa limesajili wafanyaziara milioni 15 walioingia nchini humo kwa ajili ya Arubaini ya Imam Hussein (as) huku idadi ya mazuwari hao ikiwa inaendelea kuongezeka.
-
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran aelekea Najaf Iraq kushiriki maandamano ya Arubaini
Oct 30, 2018 01:15Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo anaelekea mjini Najaf, Iraq, kwa ajili ya kushiriki katika maandamano ya Arubaini ya Imam Husain AS na pia kufanya ziara katika Haram tukufu ya Imam Ali AS.
-
Siku moja kabla ya Arubaini ya Imam Hussein (as) zaidi ya wafanyaziara milioni 10 wameshazuru Karbala
Oct 29, 2018 04:45Naibu Mkuu wa Mkoa wa Karbala nchini Iraq amesema: Hadi sasa zaidi ya wafanyaziara milioni 10 wamewasili mkoani humo kwa lengo la kushiriki Arubaini ya Imam Hussein (as).
-
Kuangamizwa ugaidi ndicho kipaumbele kikuu cha serikali mpya ya Iraq
Oct 29, 2018 01:06Jumamosi iliyopita Waziri Mkuu mpya wa Iraq, Adil Abdul-Mahdi alikutana na viongozi kadhaa wa ngazi za juu wa kijeshi na kiusalama nchini humo ambapo alisisitizia ulazima wa kuendelezwa mapambano dhidi ya makundi ya kigaidi hadi kukatwa kibisa mizizi yake.
-
Magaidi wa ISIS walijizatiti vilivyo Iraq, maghala mengine ya kemikali yagunduliwa Salahuddin, al Anbar
Oct 26, 2018 21:52Vikosi vya usalama vya Iraq vimegundua maghala mengine ya silaha za kemikali za genge la kigaidi la Daesh (ISIS) katika mikoa ya Salahuddin na al Anbar, jambo ambalo linathibitisha ni kiasi gani magaidi hao walikuwa wamejizatiti kwa silaha za kila namna hasa za kemikali na za mauaji ya umati.
-
Arubaini ya Imam Husain AS, nembo ya umoja baina ya Iran na Iraq
Oct 26, 2018 10:08Maandamano ya mamilioni ya watu katika Arubaini ya Imam Husain AS na wajibu wa kuimarishwa kadiri inavyowezekana uhusiano wa Tehran na Baghdad ndiyo ajenda kuu ya mazungumzo ya simu yaliyofanywa baina ya mawaziri wa mambo ya nje wa Iran na Iraq.
-
Kumbukumbu ya hamasa ya Arubaini ya Imam Hussein AS; nembo ya umoja wa Waislamu ulimwenguni na mshikamano wa mataifa ya Iran na Iraq
Oct 14, 2018 03:19Viongozi wa makabila yanayohamahama ya maeneo ya kusini mwa Iran na Iraq Ijumaa iliyopita walifanya mkutano katika mji wa Basra uliokuwa na nara inayosema. "Kumpenda Imam Hussein AS, Sababu ya Umoja Wetu".
-
Changamoto zinazomkabili Adil Abdul-Mahdi kwa ajili ya kuunda baraza la mawaziri nchini Iraq
Oct 09, 2018 08:31Baada ya Adil Abdul-Mahdi kuchaguliwa kuwa Waziri Mkuu wa Iraq, tayari kumeanza mazungumzo na mashauriano yenye lengo la kuunda baraza la mawaziri nchini humo.