-
Kuangamizwa DAESH kumetokana na mshikamano wa wananchi wa Syria na Iraq
Feb 20, 2018 04:42Mkuu wa Baraza Kuu la Kiislamu la Iraq amesema mshikamano wa wananchi wa nchi hiyo na wenzao wa Syria ndio uliowezesha kuangamizwa kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh katika eneo.
-
Baada ya kufanikiwa ushirikiano wao katika vita dhidi ya ugaidi, sasa Iran na Iraq zatiliana saini mapatano maalumu ya kijeshi
Feb 18, 2018 23:34Naibu Waziri wa Ulinzi wa Iran na Katibu Mkuu wa Wizara ya Ulinzi ya Iraq wamekutana na kutiliana saini mapatano maalumu ya kijeshi.
-
Saudia inalenga kuvuruga uthabiti katika eneo
Feb 18, 2018 04:00Mshauri wa Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu, Bunge la Iran, katika masuala ya kimataifa amesema Saudi Arabia inalenga kuvuruga uthabiti katika eneo kwa kuvuruga serikali zilizopo.
-
Qassemi: Al Jubeir anabwabwaja, anataka kuzungumza kwa niaba ya Wairaqi
Feb 15, 2018 12:49Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amejibu madai yaliyotolewa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia katika kikao cha kuijenga upya Iraq dhidi ya Iran na kusema: Adel al-Jubeir amesahau kwamba hawezi kuzungumza kwa niaba ya serikali ya Iraq na wananchi wa nchi hiyo.
-
Guterres: Kuijenga upya Iraq kunahitajia umoja wa kitaifa
Feb 14, 2018 13:10Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameunga mkono ubunifu wa kila namna uliotolewa kuhusu kuijenga upya Iraq na kusisitiza kuwa, ujenzi mpya wa nchi hiyo iliyoharibiwa vibaya na vita unahitajia umoja wa kitaifa kati ya watu wa matabaka yote nchini humo.
-
Nujaba ya Iraq yasema itapambana na Israel ikiiletea chokochoko Hizbullah
Feb 14, 2018 04:03Harakati ya Nujaba ya Iraq imesema itaiunga mkono kikamilifu harakati ya Hizbullah ya Lebanon iwapo italazimishwa kuingia katika vita vipya na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Wasiwasi wa Unicef kuhusu hali ya watoto wa Kiiraqi
Feb 12, 2018 10:58Mfuko wa Kuhudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (UNICEF) umetangaza kuwa mtoto mmoja wa Kiiraqi kati ya wanne nchini humo anaishi katika hali ya umaskini na kwamba Wairaqi wengine milioni nne wanahitaji msaada ikiwa ni natija ya kujiri vita vya kundi la kigaidi la Daesh huko Iraq.
-
Iraq: Saudia ilikuwa inawaruhusu magaidi kuingai nchini mwetu kuchafua usalama
Feb 11, 2018 01:10Wizara ya Ulinzi ya Iraq imetoa taarifa ikisema kuwa, utawala wa Aal-Saud nchini Saudia kuanzia mwaka 2004 hadi 2016, ilipuuza suala la kuwazuia magaidi wa Kiwahabi na wakufurishaji kuingia katika ardhi ya Iraq na kuchafua usalama.
-
Qassemi: Iran haitakubali sharti lolote lile kuhusiana na safari ya Rais wa Ufaransa mjini Tehran
Feb 05, 2018 13:01Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Tehran haitakubali sharti lolote lile kwa ajili ya safari ijayo ya Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa hapa nchini.
-
Nchi 70 kushiriki katika mkutano wa kuijenga upya Iraq
Feb 05, 2018 01:08Wizara ya Mambo ya Nje ya Iraq imetangaza kuwa, nchi 70 na mamia ya mashirika makubwa na wewekezaji wa kimataifa wametangaza nia yao ya kushiriki katika mkutano wa kuijenga upya Iraq unaotarajiwa kufanyika Kuwait baadaye mwezi huu.