-
Muungano unaoongozwa na Marekani umeua raia wasio na hatia wa Iraq
Nov 28, 2016 04:16Raia wasiopungua 18 wameuliwa katika eneo la makaazi ya raia la mji wa Mosul kaskazini mwa Iraq katika shambulio lililofanywa na muungano unaoongozwa na Marekai kwa kisingizio cha kupambana na ugaidi nchini humo.
-
Huffington Post: Arubaini ya Imam Hussein AS ni mkusanyiko mkubwa zaidi duniani
Nov 27, 2016 12:43Gazeti mashuhuri la The Huffington Post la nchini Marekani limeandika Makala kuhusu ziara ya mamilioni ya watu katika kumbukumbu ya Arubaini ya Imam Hussein AS, mjukuu wa Mtume Muhammad SAW, na kusema kuwa, huo ni mkusanyiko mkubwa zaidi wa kidini duniani.
-
Al Maliki: Uwahabi uwekwe kwenye orodha ya makundi ya kigaidi
Nov 27, 2016 02:11Waziri Mkuu wa zamani wa Iraq ametoa wito wa kuwekwa kundi la Kiwahabi katika orodha ya makundi ya kigaidi duniani.
-
Khatibu wa Sala ya Ijumaa Tehran alaani shambulio la kigaidi dhidi ya Mazuwwar nchini Iraq
Nov 25, 2016 11:49Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa mjini Tehran amelaani vikali shambulio la jana la kigaidi mjini Hilla Iraq lililopelekea kuuawa shahidi zaidi ya wafanyaziara 80 wa Imam Hussein as wakiwemo Mazuwwar 40 wa Kiirani.
-
Hizbullah yasisitiza kuendeleza mapambano dhidi ya magaidi hadi kuwaangamiza kikamilifu
Nov 25, 2016 11:41Harakati ya Mapambano ya Hizbullah ya Lebanon imesisitiza juu ya kuendeleza mapambano dhidi ya makundi ya kigaidi na kitakfiri na kuyatokomeza kikamilifu.
-
Ripoti: Genge la Daesh linawashikilia Mayazidi 3500 wa Iraq
Nov 25, 2016 04:28Kiongozi wa ofisi ya kufuatilia masuala ya raia wa Iraq wa kabila la Yazidi amesema kuwa, hadi sasa wanachama wa kundi la kigaidi la Daesh wanawashikilia mateka watu wa kabila hilo wapatao 3500.
-
Jaafari: Thuluthi moja ya Mosul imekombolewa na vikosi vya Iraq
Nov 22, 2016 04:22Waziri wa Mambo ya Nje wa Iraq amesema jeshi la nchi hiyo likishirikiana na vikosi vya kujitolea vya wananchi vimefanikiwa kukomboa thuluthi moja ya mji wa Mosul toka mikononi mwa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh.
-
Jeshi la Iraq lawatimua waandishi habari wa Saudia kutoka maeneo ya medani za kivita kwa upotoshaji
Nov 21, 2016 10:48Jeshi la Iraq limetoa amri ya kuondolewa waandishi wote wa habari wa gazeti la Asharq Al-Awsat linalochapishwa nchini Saudia kutokana na vitendo vyao vya upotoshaji na kuwavunjia heshima wanawake wa Iraq katika maeneo ya operesheni za jeshi hilo na harakati ya wananchi.
-
Jahangiri: Matembezi ya Arubaini ya Imam Hussein AS ni nembo ya amani na ukombozi
Nov 20, 2016 23:31Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, matembezi ya Arubaini ya Imam Hussein AS ni nembo ya amani na ukombozi.
-
Zaidi ya Waislamu milioni 20 waadhimisha Arubaini ya Imam Hussein, Karbalaa Iraq
Nov 20, 2016 12:44Marasimu ya kumbukumbu ya Arubaini ya Imam al-Hussein (as) mjukuu wa Mtume Muhammad (saw) yamewakutanisha pamoja Waislamu wa Kisuni na Kishia zaidi ya milioni 20 kutoka ndani na nje ya Iraq mjini Karbala.