-
Wairani waungana na dunia katika kumbukumbu ya Arubaini ya Imam Hussein AS
Nov 20, 2016 04:47Wananchi wa matabaka yote wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wameungana na dunia katika kumbukumbu ya Arubaini ya Imam Hussein AS, mjukuu wa Mtume Muhammad SAW, aliyeuawa shahidi katika jangwa la Karbala nchini Iraq, mwaka wa 61 Hijria.
-
Jeshi la Iraq lakomboa kusini mwa Mosul, magaidi 950 wauawa
Nov 19, 2016 12:13Jeshi la Iraq limetangaza kukomboa eneo la kusini mwa mji wa Mosul na kuwaangamiza magaidi zaidi ya 950 wa kundi la kitakfiri la ISIS waliokuwa wanashikilia eneo hilo.
-
Al Abadi: Wanajeshi wa Iraq wamo ndani ya mji wa Mosul hivi sasa
Nov 16, 2016 04:15Waziri Mkuu wa Iraq amesema kuwa, wanajeshi wa nchi hiyo wameshaingia katika mji wa Mosul na hivi sasa wanapambana na magaidi wa Daesh ndani ya mji huo.
-
HRW: Daesh wanatumia silaha za kemikali wakikimbia Mosul
Nov 12, 2016 04:20Shirika la kutetea haki za binadamu la Human Rights Watch limesema wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh wanatumia silaha za kemikali kaskazini mwa mji wa Mosul nchini Iraq.
-
UN: Daesh imeua makumi ya raia eneo la Hammam al-Alil, Iraq
Nov 12, 2016 00:37Umoja wa Mataifa umetangaza kuwa, kundi la kigaidi la Daesh limeua kwa umati makumi ya raia wa Iraq katika eneo la Hammam al-Alil lililoko kilomita 17 kutoka kwenye mji unaozingirwa na vikosi vya jeshi la Iraq wa Mosul.
-
Hatimaye mji wa kihistoria wa Nimrud huko Mosul wakombolewa na jeshi la Iraq kutoka kwa ISIS
Nov 10, 2016 10:09Kamanda wa operesheni za kuukomboa mji wa Mosul, makao makuu ya mkoa wa Nineve (Nainawa), kaskazini mwa Iraq, ametangaza habari ya kukombolewa mji wa kihistoria wa Nimrud ambao mwaka 2014 ulishuhudia uharibifu mkubwa wa wanachama wa genge la kigaidi la Daesh (ISIS).
-
Kaburi la umati lagunduliwa karibu na Mosul nchini Iraq
Nov 08, 2016 04:15Vikosi vya serikali ya Iraq vimegundua kaburi la umati karibu na mji wa Mosul ambao kwa sasa unashuhudia makabiliano makali kati ya vikosi hivyo na wanachama wa kundi la kigaidi na kitakfiri la Daesh/ISIS.
-
Iran yalaani mashambulizi ya kigaidi Samarra na Tikrit Iraq
Nov 07, 2016 00:47Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amelaani mashambulizi ya kigaidi yaliyopelekea watu wasiopungua 21 kuuawa katika miji ya Samarra na Tikrit nchini Iraq jana Jumapili.
-
Jeshi la Iraq laingia kaskazini mwa mji wa Mosul
Nov 06, 2016 09:46Wanajeshi wa Iraq wameingia katika eneo la kwanza kabisa la makazi ya watu kaskazini mwa mji wa Mosul, makao makuu ya mkoa wa Nainawa
-
Makumi ya maelfu ya watu waukimbia mkoa wa Nainawa, Iraq
Nov 05, 2016 23:14Kamati ya Wahajiri ya Bunge la Iraq imetangaza kuwa, karibu watu 29 elfu wameukimbia mkoa wa Nainawa tangu ilipoanza operesheni ya kuukomboa mji wa Mosul, makao makuu ya mkoa huo.