-
Spika wa Bunge la Iran atoa mwito wa kukomeshwa jinai za Israel
Jul 01, 2020 21:40Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ametoa mwito wa kuchukuliwa hatua athirifu za kukomesha jinai za utawala haramu wa Israel, hususan mpango wa utawala huo ghasibu wa kupora ardhi zaidi za Wapalestina.
-
Hania aainisha malengo matatu ya Israel ya kupora ardhi za Palestina
Jun 30, 2020 08:12Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) amesema utawala wa Kizayuni wa wa Israel unafuatilia malengo matatu makuu katika mpango wake wa kutaka kutwaa ardhi ya Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
Iran: Iwapo Israel itapora ardhi zaidi za Wapalestina itapata jibu kali la wapigania ukombozi wa Palestina
Jun 26, 2020 11:43Mshauri wa Spika wa Bunge la Iran katika masuala ya kimataifa ameuonya vikali utawala wa Kizayuni wa Israel kuhusu mpango wake wa kupora ardhi zaidi za Wapalestina katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan.
-
"Marekani kuikingia kifua Israel kumelishushia hadhi Baraza la Usalama"
Jun 25, 2020 03:19Balozi na Mwakilishi wa Kudumu wa Iran katika Umoja wa Mataifa amesema hatua ya Marekani ya kuendelea kuukingia kifua na kuunga mkono utawala wa Kizayuni wa Israel imelifanya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lipoteze hadhi yake na likose maana.
-
Jeshi la Israel latumia wanyama hai kufanyia majaribio silaha zake
Jun 22, 2020 07:44Jeshi katili la utawala wa Kizayuni wa Israel linawatumia wanyama walio hai kufanyia majaribio silaha zake kwa siri.
-
Ansarullah: Saudia na Imarati zinashirikiana na Israel dhidi ya Waislamu
Jun 19, 2020 23:33Kiongozi wa harakati ya wananchi wa Yemen ya Ansarullah amezionya vikali Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu dhidi ya kuendeleza njama za kutaka kuufanya wa kawaida uhusiano na utawala wa Kizayuni wa Israel na kusisitiza kwamba, Riyadh na Abu Dhabi zinashirikiana na Tel Aviv ambayo inajulikana ni adui mkubwa wa ulimwengu wa Kiislamu.
-
Jeshi la Lebanon lajiweka sawa baada ya askari wa Israel kwenda mpakani
Jun 19, 2020 23:27Jeshi la Lebanon limejiweka katika hali ya tahadhari baada ya kuripotiwa uwepo wa makumi ya wanajeshi wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika mpaka wa nchi hiyo ya Kiarabu na Palestina.
-
Israel kujenga 'vitongoji 300 vya Trump' katika Milima ya Golan, Syria
Jun 15, 2020 02:23Utawala ghasibu wa Israel unapanga kujenga mamia ya vitongoji vipya vya walowezi wa Kizayuni katika Miinuko ya Golan nchini Syria, vitakavyoitwa "Miinuko ya Trump".
-
Hamas yataka wanazuoni wa Kiislamu waunde kamati ya kuzima njama za Israel
Jun 14, 2020 22:41Mkuu wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (Hamas) ametoa mwito kwa wanazuoni wa Kiislamu kuunda kamati ya uratibu itakayopewa jukumu la kuunda na kutekeleza mpango wa kistratajia wa kuunga mkono kadhia ya Palestina na kukabiliana na njama za utawala wa Kizayuni wa Israel na Rais Donald Trump wa Marekani zilizopewa jina la "Muamala wa Karne."
-
Waziri wa zamani wa Misri: Israel ni adui wa kiistratajia wa Wamisri
Jun 07, 2020 22:08Waziri wa zamani wa Misri ameutaja utawala wa Kizayuni wa Israel kama adui wa kistratajia wa wananchi wa nchi hiyo ya Kiarabu ya kaskazini mwa Afrika.