-
Jeshi la Kongo laukomboa mji wa mashariki wa Uvira kutoka kwa waasi wa M23
Jan 20, 2026 07:17Vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo vimeudhibiti tena mji wa mashariki wa Uvira baada ya waasi wa kundi la M23 kuondoka katika mji huo.
-
Maporomoko ya udongo mashariki mwa Kongo yauwa takriban watu 13
Jan 14, 2026 03:07Takriban watu 13 wamepoteza maisha kufuatia maporomoko ya udongo yaliyotokea mashariki mwa Kongo mapema jana Jumanne. Watu wengien zaidi ya 30 hawajulikani waliko hadi sasa.
-
Mapigano mapya yaripotiwa kati ya vikosi vya DRC na waasi wa M23 karibu na mji muhimu wa Uvira
Jan 03, 2026 12:11Mapigano makali yamejiri leo Jumamosi kati ya waasi wa wenye silaha wa kundi la M23 na vikosi vinavyoiunga mkono serikali ya Kinshasa katika miji kadhaa karibu na mji wa Uvira, mashariki mwa DR Congo, vyanzo vya ndani vilisema.
-
DRC: Watu 1,500 wameuawa mashariki mwa nchi
Jan 02, 2026 02:47Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imesema zaidi ya raia 1,500 wameuawa katika ghasia zinazoendelea katika jimbo la Kivu Kusini, mashariki mwa nchi hiyo tangu mapema mwezi Desemba, 2025 mpaka sasa.
-
Ukatili wa kingono dhidi ya watoto nchini Kongo umekithiri na ni wa kimfumo
Jan 01, 2026 02:25Ukatili wa kingono dhidi ya watoto limekuwa jambo la kawaida, la kimfumo na unazidi kuongezeka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Hii ni kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF).
-
Msimamo wa Uingereza dhidi ya wahamiaji wa DRC; kwa nini London inashadidisha mashinikizo dhidi ya nchi za Kiafrika?
Dec 29, 2025 06:58Uingereza imeibua wimbi kubwa la mijibizo na malalamiko ya ndani na ya kimataifa kwa hatua yake ya kuweka vizuizi vya viza na kupitisha mageuzi makali kwa utoaji hifadhi ya ukimbizi.
-
Waasi wa M23 wamebaki Uvira licha ya kutangaza kuwa tayari kuondoka katika mji huo
Dec 18, 2025 07:25Waasi wa kundi la M23 hawajaondoka katika mji wa Uvira mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo licha ya mapema wiki hii kutangaza kuwa wataondoka katika mji huo.
-
M23 yaendelea kuwashikilia mamia ya askari wa Burundi
Dec 16, 2025 04:06Kundi la waasi wa M23 linalodaiwa kuungwa mkono na Rwanda limewakamata mamia ya wanajeshi wa Burundi wakati wa mashambulizi yake ya hivi punde mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, afisa wa kundi hilo amesema, huku mapigano yakiendelea mashariki mwa DRC.
-
Serikali ya Kongo yatoa hakikisho; yasema haitasalimu amri licha ya hali ya wasiwasi mashariki mwa nchi
Dec 13, 2025 09:52Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo jana Ijumaa ilitoa hakikisho ikieleza kuwa jeshi la nchi hiyo halitasalimu amri" kufuatia kutekwa mji wa Uvira.
-
Waasi wa M23 wadai kuuteka mji wa kiistratejia wa Uvira, mashariki mwa Kongo
Dec 11, 2025 11:58Waasi wa M23 katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo jana Jumatano walitoa taarifa wakidai kuuteka mji wa kimkakati wa Uvira, ambao ni kitovu muhimu cha kibiashara karibu na mpaka wa nchi hiyo na Burundi.