Jul 17, 2020 08:05
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameashiria juu ya makubaliano ya miaka 25 ya ushirikiano kati ya Iran na China na kusisitiza kuwa, katu Jamhuri ya Kiislamu haitapeana hata shibri moja ya ardhi yake au kuipa nchi yoyote ile ikiwemo China, haki maalumu ya kutumia maeneo yake.