-
Kwa mara nyingine Ujerumani yaihimiza Ulaya kuitenga Marekani katika mfumo wa fedha
Sep 01, 2018 02:53Kwa mara nyingine tena, Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumiani amezihimiza nchi za Ulaya kutafuta njia za kuwa na mfumo wao wa kujitegemea wa kifedha kama njia ya kudumisha mapatano ya nyuklia na Iran yanayojulikana kwa kifupi kama JCPOA.
-
IAEA yathibitisha kwa mara ya 12 kuwa Iran imeheshimu kikamilifu mapatano ya JCPOA
Aug 30, 2018 23:23Kazem Gharib Abadi, balozi na mwakilishi wa kudumu wa Iran katika mashirika ya kimataifa yenye makao yao mjini Vienna, Austria amesema kuwa, kwa mara ya 12 mtawalia, Wakala wa Kimataifa wa Nishati ya Atomiki IAEA umethibitisha kuwa Iran imeheshimu kikamilifu mapatano ya nyuklia ya JCPOA.
-
Rouhani: Wanachama wa JCPOA wanapaswa kutekeleza haraka mipango yao ya kulinda makubaliano hayo
Aug 27, 2018 10:21Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amefanya mazungumzo ya simu na mwenzake wa Ufaransa na kusema kuwa, kwa kutilia maanani hatua ya Marekani ya kujiondoa katika makubaliano ya nyuklia ya JCPOA, nchi nyingine wanachama katika mapatano hayo zinapaswa kutekeleza mipango yao haraka na kwa uwazi kwa ajili ya kulinda makubaliano hayo.
-
Zarif: Viongozi wa Marekani wameelekeza zaidi fikra zao katika vita vya kisaikolojia
Aug 26, 2018 03:00Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa viongozi wa Marekani wameelekeza zaidi fikra zao katika vita vya kisaikolojia huku wakifanya juhudi za kuzidisha mashinikizo ya kisaikolojia dhidi ya Wairani na washirika wa kimataifa wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Makubaliano ya JCPOA yataendelea kutekelezwa bila ya Marekani
Aug 20, 2018 03:18Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema Marekani imekuwa mraibu wa uwekaji vikwazo na kusisitiza kwamba makubaliano ya nyuklia ya JCPOA yataendelea kutekelezwa hata bila ya kushiriki Marekani.
-
Russia, China zasisitiza kulinda mapatano ya nyuklia ya Iran
Aug 18, 2018 02:48Russia na China zimesistiza kuwa zitaendelea kufungamana na mapatano ya nyuklia ya Iran ya mwaka 2015 yanayojulikana kama Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezwaji, JCPOA.
-
London yakataa matakwa ya Marekani ya kuiwekea vikwazo Iran
Aug 17, 2018 02:41Wizara ya Mambo ya Nje ya Uingereza imekataa wito wa Marekani wa kujiunga na Washington katika vikwazo vyake vipya dhidi ya Iran.
-
Tehran: Marekani inapaswa kuliomba radhi rasmi taifa la Iran
Aug 09, 2018 23:23Waziri wa Mambo wa Ndani ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Marekani inapaswa kuheshimu ahadi zake katika mapatano ya nyuklia ya JCPOA na iliombe radhi rasmi taifa la Iran.
-
Qassemi: Hakuna imani yoyote ya kufanya mazungumzo na Marekani
Aug 07, 2018 10:08Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuhusu matamshi ya karibuni ya rais wa Marekani kuwa yuko tayari kufanya mazungumzo na viongozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kwamba: kutokana na sera za Marekani za kuendesha vita vikubwa vya kisaikolojia dhidi ya Iran hakuna dhamana wala imani yoyote juu ya serikali ya Marekani wala rais wa nchi hiyo.
-
Nchi za Ulaya zapinga vikwazo vya Marekani dhidi ya Iran
Aug 07, 2018 10:06Nchi za Ulaya zimetangaza kupinga vikwazo vipya vya Marekani dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sambamba na kutangaza kuunga mkono mapatano ya nyuklia maarufu kama JCPOA.