Feb 21, 2019 02:55
Waziri wa Ulinzi wa Venezuela ametangaza tena utiifu wake na vikosi vya majeshi ya nchi hiyo kwa Rais Nicolas Maduro wa nchi hiyo na kusema kuwa, makamanda na wanajeshi wa nchi hiyo wanafuata na kuutii amri ya Rais Maduro na wataendelea kusimama naye bega kwa bega hadi tone la mwisho la damu yao.