Nov 29, 2018 07:15
Ayatullah Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa vikosi vyote vya ulinzi vya Iran jana alikutana na makamanda na wakuu wa Jeshi la Majini la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kusema kumepatikana mafanikio makubwa katika Jeshi la Iran hasa jeshi la majini tokea mwanzo wa Mapinduzi ya Kiislamu hadi sasa.