Jun 04, 2020 12:41
Maandamano makubwa ambayo hayajawahi kutokea mfano wake huko Marekani yamemtia kiwewe na kumuweka kwenye hali ngumu rais wa nchi hiyo mwenye majigambo na majivuno mengi, Donald Trump na kumfanya atoe amri ya kutumiwa jeshi, suala ambalo limelalamikiwa na Wizara ya Ulinzi, lakini hata wanachama wenzake ndani ya chama cha Republican nao hawakubaliani na uamuzi wake wa kutumia nguvu za kijeshi kukandamiza waandamanaji.