Nov 25, 2023 07:02
Kaimu Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) amesema kuwa, nguvu zilizooneshwa na wananchi wa Palestina katika vita vya hivi sasa vya Ghaza zimeishangaza dunia na kuifanya iemewe, na ijiulize, nguvu hizi wamezitoa wapi wananchi hawa wa Palestina.