-
Bunge la 11 la Iran lafunguliwa kwa hotuba ya Kiongozi Muadhamu
May 27, 2020 03:32Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amelitaka Bunge la 11 la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran lililoanza shughuli zake leo Jumatano kuelekeza darubini na kujikita zaidi katika masuala ya uchumi wa kimuqawama na utamaduni.
-
PFLP: Hotuba ya Kiongozi Muadhamu imeainisha ramani ya njia ya kuikomboa Palestina
May 23, 2020 03:36Afisa wa ngazi za juu wa Palestina amesema hotuba ya jana ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Quds imechora na kuanisha ramani ya njia ya ukombozi wa Palestina.
-
Kiongozi Muadhamu: Tutaliunga mkono taifa lolote linalopambana na utawala wa Kizayuni
May 21, 2020 03:22Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran italiunga mkono taifa lolote lile linalosimama kidete dhidi ya utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Mtazamo wa Kiongozi Muadhamu; Uzalishaji, msingi wa kujengea uchumi imara
May 07, 2020 03:37Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema, uzalishaji ndio msingi unaowezesha kupatikana uchumi wa kitaifa na ulio imara.
-
Kiongozi Muadhamu asisitiza kuhusu umuhimu wa wafanyakazi katika uchumi salama
May 06, 2020 07:02Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuhusu nafasi na umuhimu wa wafanyakazi na majukumu ya mwajiri na mwajiriwa katika kuimarisha ubora na wingi wa uzalishaji na utajiri katika uchumi salama.
-
Kiongozi Muadhamu atuma salamu za kuenzi Siku ya Mwalimu nchini Iran
May 01, 2020 09:16Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma salamu za mkono wa kheri na baraka kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Mwalimu nchini Iran na kusema kuwa walimu wote, maskulini, vyuoni na katika Hawza (Chuo Kikuu cha Kidini) wanafanya kazi kubwa ya kulea vipaji vya watoto na mabarobaro katika njia ya matukufu ya Kiislamu na Kimapinduzi kwa shabaha ya kuunda jamii ya kidini, yenye uadilifu na yenye malengo makuu matukufu.
-
Kiongozi Muadhamu: Iran ina nafasi muhimu katika kudhamini usalama wa Ghuba ya Uajemi
Apr 30, 2020 03:46Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina nafasi muhimu katika kuhakikisha kuwa usalama unakuwepo katika eneo la Ghuba ya Uajemi.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi kuhusu udharura wa kutowaogopa maadui wa Uislamu na madola dhalimu
Apr 26, 2020 02:51Njia pekee ya kuinusuru jamii ya wanadamu kuondokana na dhulma, ubaguzi, maonevu, vita, ukosefu wa usalama, na kutoheshimiwa thamani za kiutu ambako kumeshuhudiwa katika kipindi chote cha historia, ni kufuata kivitendo mafundisho ya Qurani Tukufu.
-
Kiongozi Muadhamu: Hitajio la mwanadamu wa leo kwa mkombozi ni nadra kuwahi kushuhudiwa katika historia
Apr 09, 2020 08:41Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema hitajio la kina na pana la mwanadamu wa leo la kuwa na mkombozi ni nadra kushuhudiwa katika historia. Amesisitiza kuwa, maana halisi na yenye manufaa ya kusubiri mwokozi ni kuwa na matumaini na itikadi kuhusu faraja sambamba na kuchukua hatua za kufikia mustakbali mwema na akaongeza kuwa: "Taifa la Iran limefaulu vizuri katika mtihani wa ugonjwa wa hivi karibuni; na mwenendo na nidhamu ya umma ni nzuri katika kufuata maelekezo."
-
Kiongozi Muadhamu alipongeza taifa la Iran kwa kukabiliana na janga la corona
Apr 09, 2020 03:53Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amelipongeza taifa la Iran kwa jitihada zake za dhati za kupambana na ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya corona, huku akilitaja janga hilo kama mtihani unaoikabili dunia nzima.