-
Kiongozi Muadhamu asisitiza kuhusu umuhimu wa wafanyakazi katika uchumi salama
May 06, 2020 11:32Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuhusu nafasi na umuhimu wa wafanyakazi na majukumu ya mwajiri na mwajiriwa katika kuimarisha ubora na wingi wa uzalishaji na utajiri katika uchumi salama.
-
Kiongozi Muadhamu atuma salamu za kuenzi Siku ya Mwalimu nchini Iran
May 01, 2020 13:46Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametuma salamu za mkono wa kheri na baraka kwa mnasaba wa maadhimisho ya Siku ya Mwalimu nchini Iran na kusema kuwa walimu wote, maskulini, vyuoni na katika Hawza (Chuo Kikuu cha Kidini) wanafanya kazi kubwa ya kulea vipaji vya watoto na mabarobaro katika njia ya matukufu ya Kiislamu na Kimapinduzi kwa shabaha ya kuunda jamii ya kidini, yenye uadilifu na yenye malengo makuu matukufu.
-
Kiongozi Muadhamu: Iran ina nafasi muhimu katika kudhamini usalama wa Ghuba ya Uajemi
Apr 30, 2020 08:16Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ina nafasi muhimu katika kuhakikisha kuwa usalama unakuwepo katika eneo la Ghuba ya Uajemi.
-
Sisitizo la Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi kuhusu udharura wa kutowaogopa maadui wa Uislamu na madola dhalimu
Apr 26, 2020 07:21Njia pekee ya kuinusuru jamii ya wanadamu kuondokana na dhulma, ubaguzi, maonevu, vita, ukosefu wa usalama, na kutoheshimiwa thamani za kiutu ambako kumeshuhudiwa katika kipindi chote cha historia, ni kufuata kivitendo mafundisho ya Qurani Tukufu.
-
Kiongozi Muadhamu: Hitajio la mwanadamu wa leo kwa mkombozi ni nadra kuwahi kushuhudiwa katika historia
Apr 09, 2020 13:11Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema hitajio la kina na pana la mwanadamu wa leo la kuwa na mkombozi ni nadra kushuhudiwa katika historia. Amesisitiza kuwa, maana halisi na yenye manufaa ya kusubiri mwokozi ni kuwa na matumaini na itikadi kuhusu faraja sambamba na kuchukua hatua za kufikia mustakbali mwema na akaongeza kuwa: "Taifa la Iran limefaulu vizuri katika mtihani wa ugonjwa wa hivi karibuni; na mwenendo na nidhamu ya umma ni nzuri katika kufuata maelekezo."
-
Kiongozi Muadhamu alipongeza taifa la Iran kwa kukabiliana na janga la corona
Apr 09, 2020 08:23Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amelipongeza taifa la Iran kwa jitihada zake za dhati za kupambana na ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya corona, huku akilitaja janga hilo kama mtihani unaoikabili dunia nzima.
-
Katika siku ya kuzaliwa Abul Fadh'l: Ayatullah Khamenei awapongeza vilema wa vita, awataja kuwa ni mashahidi walio hai
Mar 29, 2020 10:36Sambamba na maadhimisho ya siku ya kuzaliwa Abul Fadh'li Abbas bin Ali bin Abi Twalib (as), na Siku ya Wenye Kijitoa Mhanga, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei ametoa taarifa akipongeza nafasi na mchango wa vilema wa vita wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran.
-
Kiongozi Muadhamu: India isitishe mauaji ya Waislamu iwapo haitaki kutengwa
Mar 05, 2020 13:25Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameitahadharisha serikali ya India dhidi ya kuendelea kutekeleza mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wa nchi hiyo na kusisitiza kuwa, ukandamizaji unaoendelea kufanyiwa Waislamu katika nchi hiyo ya kusini mwa Asia utapelekea serikali ya New Delhi itengwe katika ulimwengu wa Kiislamu.
-
Baraza la Mamufti Russia lamshukuru Kiongozi Muadhamu kwa kuwatetea Wapalestina
Mar 01, 2020 08:09Baraza la Mamufti la Russia limempongeza na kumshukuru Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Ali Khamenei kwa kutetea haki halali za Wapalestina.
-
Kiongozi Muadhamu apongeza jitihada za wahudumu wa afya nchini za kupambana na Corona
Feb 27, 2020 13:04Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amepongeza jitihada zinazofanywa na maafisa na wahudumu wa afya hapa nchini kwa ajili ya kupambana na virusi vya Corona.