-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Uingereza ni chanzo cha vitisho Asia Magharibi
Dec 18, 2016 04:37Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu jana Jumamosi alihutubia kikao cha Maulidi ya Mtume Muhammad (saw) kilichohudhuriwa na viongozi wa Iran, wageni wanaoshiriki katika Mkutano wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu, mabalozi wa nchi za Kiislamu na watu wa matabaka mbalimbali na kusisitiza kuwa, katika siku chache zilizopita Waingereza na bila ya kuona aibu, waliitaja Iran kuwa ni tishio la eneo la Ghuba ya Uajemi ilhali nchi hiyo ndiyo chanzo cha vitisho, ufisadi na hatari za aina mbalimbali.
-
Kiongozi Muadhamu: Uingereza daima ni chimbuko la vitisho, ufisadi na mabalaa magharibia mwa Asia
Dec 17, 2016 17:14Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, daima Uingereza imekuwa chimbuko la vitisho, ufisadi na mabalaa kwa eneo la magharibi mwa Asia.
-
Kiongozi Muadhamu: Mapigano magharibi mwa Asia ni ya kutwishwa
Dec 15, 2016 04:37Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, machafuko yanayoshuhudiwa katika eneo la magharibi mwa Asia ni ya kutwishwa na ni kwa mujibu wa malengo ya kikhabithi kutoka nje.
-
Kiongozi Muadhamu: Palestina itakombolwewa kwa baraka za mapambano ya Wapalestina
Dec 14, 2016 14:32Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: "Pamoja na kuwa waitifaki wa utawala wa Kizayuni wanaibua migogoro mara kwa mara ili kadhia ya Palestina isahaulike, lakini ardhi hii takatifu itakombolewa kwa baraka za muqawama na jihadi ya taifa na makundi ya Palestina".
-
Kiongozi Muadhamu: Adui anafanya njama za kujipenyeza kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni nchini Iran
Dec 14, 2016 04:29Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema, moja ya malengo makuu ya adui ni kujipenyeza kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni nchini Iran na anawalenga zaidi vijana na mabarobaro wa taifa hili la Kiislamu.
-
Kiongozi Muadhamu: Kuendeleza vikwazo dhidi ya Iran ni kinyume na JCPOA
Nov 23, 2016 15:20Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, hatua ya kurefusha vikwazo dhidi ya Iran kwa miaka 10 zaidi, bila ya shaka yoyote ni uvunjaji wa makubaliano ya nyuklia yanayojulikana kwa jina maarufu la JCPOA.
-
Kiongozi: Makundi ya kigaidi kama ISIS yametokana na uingiliaji wa madola makubwa
Nov 22, 2016 17:02Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ameashiria matukio machungu na ya kusikitisha katika eneo na nafasi ya baadhi ya madola makubwa katika kulazimisha ukosefu wa uthabiti na vita katika mataifa na kusistiza kuwa: "Jamhuri ya Kiislamu ya Iran daima imekuwa ikitoa wito kwa nchi zenye misimamo huru kuwa na nafasi yenye harakati katika kukabiliana na mashinikizo dhidi ya mataifa na inayataka yasikae kimya na kuwa watazamaji."
-
Ayatullah Khamenei: Iran haina hukumu yoyote kuhusu uchaguzi wa Marekani
Nov 16, 2016 14:25Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haina hukumu ya aina yoyote kuhusu uchaguzi wa rais wa Marekani na kuongeza kuwa, Iran daima imekuwa ikishuhudia uadui kutoka kwa vyama viwili vikuu vya Marekani.
-
Kiongozi Muadhamu: Muungano wa Magharibi hauna nia ya kweli ya kuutokomeza ugaidi
Oct 25, 2016 16:44Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema nchi zenye misimamo huru zinapaswa kuimarisha uhusiano baina yao na kutoathiriwa na siasa za madola ya Kiistikbari ili kuweza kuzima moto wa hitilafu na mapigano uliowashwa na madola hayo.
-
Kiongozi: Ni marufuku kwa Serikali, Bunge, Mahakama, vikosi vya ulinzi, kuingilia uchaguzi Iran
Oct 15, 2016 15:58Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ametumia haki yake aliyopewa na kifungu nambari 110 cha Katiba, kuwasilisha siasa kuu za uchaguzi baada ya kushauriana na Halmashauri ya Kuainisha Maslahi Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.