-
Ayatullah Khamenei amjibu Trump: Iran haimuogopi yeyote, Marekani isubiri majibu 10 Februari
Feb 07, 2017 10:05Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa taifa la Iran litajibu vitisho vilivyotolewa na Rais Donald Trump wa Marekani katika maadhimisho ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran Ijumaa ijayo.
-
Rais Rouhani: Ayatullah Rafsanjani alikuwa msaidizi imara wa Kiongozi Muadhamu
Jan 16, 2017 04:02Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema: "Kuaga dunia Ayatullah Hashemi Rafsanjani aliyekuwa Mkuu wa Halmashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Kiislamu wa Iran, ni msiba mkubwa ambao umepelekea Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu kupoteza tegemeo lake kubwa."
-
Ayatullah Rafsanjani kuzikwa leo, Swala ya maiti inaongozwa na Ayatullah Ali Khamenei
Jan 10, 2017 01:05Ofisi ya Hamlashauri ya Kuainisha Maslahi ya Mfumo wa Kiislamu nchini Iran imetangaza kuwa, mwili wa marehemu Ayatullah Akbar Hashemi Rafsanjani utazikwa leo baada ya Swala ya maiti itakayoongozwa na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullahil Udhmaa Ali Khamenei.
-
Kiongozi: Ni lazima Iran iimarishe uwezo wake
Dec 27, 2016 11:08Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatollah Ali Khamenei amesema Iran inapaswa kuendelea kuimarisha nguvu zake ili kukabiliana na aina mbali mbali za maadui.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Uingereza ni chanzo cha vitisho Asia Magharibi
Dec 18, 2016 01:07Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu jana Jumamosi alihutubia kikao cha Maulidi ya Mtume Muhammad (saw) kilichohudhuriwa na viongozi wa Iran, wageni wanaoshiriki katika Mkutano wa Kimataifa wa Umoja wa Kiislamu, mabalozi wa nchi za Kiislamu na watu wa matabaka mbalimbali na kusisitiza kuwa, katika siku chache zilizopita Waingereza na bila ya kuona aibu, waliitaja Iran kuwa ni tishio la eneo la Ghuba ya Uajemi ilhali nchi hiyo ndiyo chanzo cha vitisho, ufisadi na hatari za aina mbalimbali.
-
Kiongozi Muadhamu: Uingereza daima ni chimbuko la vitisho, ufisadi na mabalaa magharibia mwa Asia
Dec 17, 2016 13:44Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesisitiza kuwa, daima Uingereza imekuwa chimbuko la vitisho, ufisadi na mabalaa kwa eneo la magharibi mwa Asia.
-
Kiongozi Muadhamu: Mapigano magharibi mwa Asia ni ya kutwishwa
Dec 15, 2016 01:07Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa, machafuko yanayoshuhudiwa katika eneo la magharibi mwa Asia ni ya kutwishwa na ni kwa mujibu wa malengo ya kikhabithi kutoka nje.
-
Kiongozi Muadhamu: Palestina itakombolwewa kwa baraka za mapambano ya Wapalestina
Dec 14, 2016 11:02Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: "Pamoja na kuwa waitifaki wa utawala wa Kizayuni wanaibua migogoro mara kwa mara ili kadhia ya Palestina isahaulike, lakini ardhi hii takatifu itakombolewa kwa baraka za muqawama na jihadi ya taifa na makundi ya Palestina".
-
Kiongozi Muadhamu: Adui anafanya njama za kujipenyeza kisiasa, kiuchumi, kiutamaduni nchini Iran
Dec 14, 2016 00:59Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema, moja ya malengo makuu ya adui ni kujipenyeza kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni nchini Iran na anawalenga zaidi vijana na mabarobaro wa taifa hili la Kiislamu.
-
Kiongozi Muadhamu: Kuendeleza vikwazo dhidi ya Iran ni kinyume na JCPOA
Nov 23, 2016 11:50Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, hatua ya kurefusha vikwazo dhidi ya Iran kwa miaka 10 zaidi, bila ya shaka yoyote ni uvunjaji wa makubaliano ya nyuklia yanayojulikana kwa jina maarufu la JCPOA.