-
Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) awasili mjini Beirut, Lebanon
Oct 12, 2024 11:48Mohammad Bagher Ghalibaf Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) ambaye yupo njiani kuelekea Geneva kushiriki Mkutano wa Kilele wa Mabunge ya Dunia, amewasili mjini Beirut kabla ya kuelekea Uswisi kwa ajili ya kuonana na kuzungumza na viongozi wa Lebanon na kutangaza uungaji mkono wake kwa Harakati ya Muqawama ya Hizbullah ya Lebanon.
-
Iran: Tumejiweka tayari kikamilifu kulinda mamlaka ya utawala ya ardhi yetu
Oct 11, 2024 07:46Balozi na mwakilishi wa kudumu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa amesisitiza kuwa, Jamhuri ya Kiislamu imejiweka tayari kikamilifu kulinda mamlaka yake na umoja wa ardhi yake dhidi ya uvamizi na uchokozi wowote utakaoyalenga maslahi yake makuu na usalama wake.
-
Unicef: Watoto zaidi ya 100 wameuawa Lebanon katika siku 11
Oct 06, 2024 11:06Mfuko wa Kuwahudumia Watoto wa Umoja wa Mataifa (Unicef) umetangaza kuwa watoto zaidi ya 100 wameuawa huko Lebanon siku 11 zilizopita kufuatia hujuma na mashambulizi yanayoendelea kufanywa na jeshi la Israel nchini humo.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran: Usitishaji vita Lebanon na Gaza unapaswa kufanyika kwa wakati mmoja
Oct 05, 2024 02:34Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa, Iran inaunga mkono usitishaji vita kwa sharti kwamba, haki za wananchi wa Lebanon ziheshimiwe na kukubaliwa na Muqawama na kusema: Usitishaji huo wa mapigano unapaswa kuwa sawia na usitishaji vita huko Gaza.
-
Israel yaendelea kumwaga damu za Walebanon mjini Beirut
Oct 04, 2024 07:13Wizara ya Afya ya Lebanon imesema takriban watu 37 wameuawa shahidi huku wengine zaidi ya 150 wakijeruhiwa katika mashambulizi mapya ya anga ya utawala haramu wa Israel, huku uchokozi usio na kikomo wa utawala huo katili dhidi ya Lebanon ukiendelea.
-
UNICEF yaeleza wasiwasi wake kuhusu hali mbaya ya watoto wa Lebanon
Oct 01, 2024 13:46Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF, ametahadharisha kuhusu hali mbaya ya kibinadamu nchini Lebanon na ameelezea wasiwasi wake kuhusu hali ya watoto nchini humo.
-
Madai ya Marekani katika muktadha wa kujaribu kuzuia vita Asia Magharibi
Oct 01, 2024 02:17Marekani ambayo ni mdhamini mkubwa zaidi wa silaha kwa utawala wa Kizayuni wa Israel kwa ajili ya mashambulizi makubwa dhidi ya watu wa Lebanon na Gaza, sasa inajitokeza kwa unafiki na kutoa wito wa kupunguzwa mivutano na kurejeshwa amani katika eneo la Magharibi mwa Asia.
-
Abu Sharif: Irada ya muqawama ina nguvu kuliko njama yoyote
Sep 30, 2024 12:01Mwakilishi wa Harakati ya Jihad Islami ya Palestina amesema baada ya utawalal wa Kizayuni kumuua shahidi Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon kwamba: Licha ya kuipoteza nembo hiyo adhimu, lakini si tu muqawama hautadhoofishwa bali utaendeleza njia yake kwa nguvu zaidi na kwa azma kamili.
-
Utawala wa Kizayuni waua kigaidi makamanda 3 wa chama cha PLO
Sep 30, 2024 07:57Shambulio la kigaidi ambalo limetekelezwa na utawala wa Kizayuni katika eneo la "Al-Kola" mjini Beirut, Lebanon limepelekea kuuawa shahidi makamanda watatu waandamizi wa chama cha Ukombozi wa Palestina PLO.
-
SEPAH: Malengo matukufu ya ukombozi wa Quds yamekaribia kufikiwa
Sep 29, 2024 06:10Kamanda Mkuu wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (SEPAH) ametoa ujumbe maalumu wa pongezi na wa mkono wa pole kufuatia kuuawa shahidi Sayyid Hassan Nasrullah, Katibu Mkuu wa Hizbullah ya Lebanon na kusisitiza kuwa, malengo matukufu ya ukombozi wa Quds yamekaribia kufikiwa na historia itathibitisha hilo.