-
Mjumbe mpya wa Umoja wa Mataifa kuhusu Libya aanza kazi rasmi
Feb 08, 2021 12:07Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Libya leo Jumatatu, Februari 8, 2021 ameanza kazi rasmi.
-
Waziri Mkuu mpya wa Libya apewa siku 21 kuunda serikali
Feb 06, 2021 10:22Waziri Mkuu mpya wa Libya amepewa siku 21 kuwa ametangaza serikali mpya baada ya kupasishwa kwa wingi wa kura za baraza la mazungumzo ya amani ya Libya.
-
Menfi achaguliwa rais wa muda nchini Libya, al-Dabaiba waziri mkuu
Feb 06, 2021 01:16Mohammed al-Menfi amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa Baraza la Urais la Libya huku Abdulhamid al-Dabaiba akichaguliwa kuwa waziri mkuu katika zoezi ambalo limesimamiwa na Umoja wa Mataifa siku ya Ijumaa. Wajumbe kutoka kambi hasimu nchini Libya wameafiki kunda serikali hiyo ya mpito katika kikao ambacho kimefanyika karibu na mji wa Geneva nchini Uswisi.
-
Wanamgambo wa Haftar wapigana wao kwa wao katika mji wa Sirte, Libya
Feb 02, 2021 07:46Duru za habari zimearifu kuwa, wanamgambo wanaoongozwa na Jenerali muasi Khalifa Haftar kamanda wa vikosi kwa jina la jeshi la kitaifa la Libya wamepigana wao kwa wao katika mji wa Sirte huko Libya.
-
Wagombea wa Baraza la Urais la Libya watangazwa
Jan 31, 2021 04:13Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya ametangaza orodha ya wagombea wa Baraza la Urais na kiti cha Waziri Mkuu nchini humo.
-
Maiti 139 zagunduliwa katika makaburi ya umati Libya
Jan 23, 2021 08:22Jumla ya maiti 139 zimegunduliwa katika makaburi ya umati katika mji wa Tarhauna, magharibi mwa Libya tokea mwezi Juni mwaka uliopita 2020 hadi sasa.
-
Umoja wa Mataifa watangaza tarehe ya uchaguzi wa Serikali ya Mpito Libya
Jan 22, 2021 08:23Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Libya umetangaza kuwa, wagombea wa nafasi za uongozi katika serikali mpya ya mpito ya Libya wanatakiwa wajulikane katika kipindi cha wiki moja ijayo ili mwanzoni mwa mwezi ujao wa Februari kupigwe kura ya kuwachagua wagombea hao.
-
Misri yakaribisha mapatano ya Libya kuhusu mchakato wa katiba ya nchi hiyo
Jan 21, 2021 08:23Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri imekaribisha mapatano yaliyofikiwa na pande za Libya kuhusu mchakato wa katiba ya nchi hiyo.
-
UN yatoa wito wa kurejeshwa operesheni za uokozi baada ya wahajiri 43 kupoteza maisha
Jan 21, 2021 04:11Mashirika ya Umoja wa Mataifa ya uhamiaji IOM na lile la kuhudumia wakimbizi UNHCR yametoa wito kwa nchi kurejesha operesheni za kuwasaka na kuwaokoa watu kwenye bahari ya Mediterania baada ya wahajiri wengine 43 kupoteza maisha katika ajali ya boti iliyotokea siku ya Jumatatu katika pwani ya Libya.
-
Mkuu wa UN ataka askari ajinabi waondoke Libya haraka iwezekavyo
Jan 19, 2021 08:27Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametaka wanajeshi na mamluki wote wa nchi ajinabi waondoke nchini Libya haraka iwezekanavyo.