Wagombea wa Baraza la Urais la Libya watangazwa
https://parstoday.ir/sw/news/africa-i66302-wagombea_wa_baraza_la_urais_la_libya_watangazwa
Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya ametangaza orodha ya wagombea wa Baraza la Urais na kiti cha Waziri Mkuu nchini humo.
(last modified 2023-11-27T12:14:11+00:00 )
Jan 31, 2021 07:43 UTC
  • Wagombea wa Baraza la Urais la Libya watangazwa

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya ametangaza orodha ya wagombea wa Baraza la Urais na kiti cha Waziri Mkuu nchini humo.

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Libya ametangaza orodha ya wagombea wa baraza la kiti cha urais ambayo ndani yake kunaonekana baadhi ya majina kama ya Khaled Ammar Al-Misri, Agila Saleh Qwaider na Salahuddin Al-Namroush; huku Ahmed Omar Ahmed Meitig, Osama Al-Sayd na Fathi Ali Abdul Salam Bashagha wakiarifishwa pia  miongoni mwa wagombea wa  nafasi ya Waziri Mkuu huko Libya.  

Aguila Saleh, ni kati ya wagombea waliotangazwa wa kiti cha urais huko Libya

Libya imekuwa ikikabiliwa na machafuko na ukosefu wa amani tangu kupinduliwa madarakani utawala wa kidikta wa Kanali Muammar Gaddafi mwaka 2011. 

Weledi wa mambo wanaamini kuwa njia pekee ya kuhitimisha mgogoro wa Libya ni kufanyika uchaguzi na kuundwa serikali na jeshi lenye nguvu nchini humo.  

Kwa kuzingatia hali ya mambo ilivyo huko Libya takwa kuu la wananchi pia ni kufanyika uchaguzi ambao utapelekea kuingia madarakani serikali yenye nguvu ili kuhitimisha hali mbaya ya sasa nchini humo.