-
Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa Libya: Tunakaribia kupata ushindi mkubwa
May 19, 2020 10:53Kiongozi wa Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya (GNA) Fayez al-Sarraj amesisitiza kuwa vikosi vya serikali yake vinakaribia kupata ushindi mkubwa baada ya kukikomboa kituo cha anga cha al-Watiya kilichoko magharibi mwa mji mkuu wa nchi hiyo,Tripoli.
-
Jeshi la Libya lachukua udhibiti wa uwanja wa ndege za kijeshi kutoka wapiganaji wa Haftar
May 18, 2020 06:13Jeshi la Libya leo Jumatatu limechukua udhibiti wa Uwanja wa Ndege za Kijeshi wa Al-Watiya kutoka kwa wapiganaji wa jenerali muasi Khalifa Haftar
-
Ujerumani yalaumiwa kwa kutumia vibaya mgogoro wa Libya
May 17, 2020 20:11Duru mbalimbali duniani zinailaumu Ujerumani kwa kuchochea mapigano nchini Libya na kutojali vikwazo na marufuku ya kutopeleka silaha katika nchi hiyo iliyoathiriwa vibaya na vita.
-
Serikali ya mwafaka wa kitaifa ya Libya yataka kukatwa uhusiano na Imarati
May 16, 2020 06:32Mjumbe wa Baraza la Rais la Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa nchini Libya, sambamba na kuashiria ripoti ya siri ya Umoja wa Mataifa kuhusiana na uungaji mkono wa Imarati kwa jenerali muasi Khalifa Haftar, ametaka kukatwa uhusiano wa Tripoli na Abu Dhabi.
-
Kupamba moto mgogoro Libya na uingiliaji wa maajinabi katika masuala ya ndani ya nchi hiyo
May 13, 2020 07:14Mapigano ya ndani nchini Libya yamepamba moto hivi sasa na kutoa fursa kwa madola ajinabi yanayojali maslahi yao binafsi tu, kuingilia masuala ya ndani ya nchi hiyo.
-
Onyo la Uturuki dhidi ya vikosi vyenye mfungamano na Saudi Arabia nchini Libya
May 12, 2020 05:37Uwepo wa kijeshi wa Uturuki nchini Libya na vita vya niaba vya Ankara dhidi ya baadhi ya madola ya Kiarabu yenye fikra mgando kama Saudi Arabia, kumeshadidisha matatizo ya serikali ya Recep Tayyip Erdogan barani Afrika.
-
Uturuki: Taarifa ya nchi tano dhidi yetu imetumia vipimo vya kiundumakuwili
May 12, 2020 03:10Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki imesema, taarifa ya pamoja iliyotolewa na Misri, Ugiriki, Imarati, Ufaransa na Cyprus kuhusu Bahari ya Mediterania inaonyesha vipimo vya kiundumakuwili vinavyotumiwa na nchi hizo.
-
Spika wa Bunge la Libya: Khalifa Haftar hatokuwa mshirika wetu wa kisiasa hapo baadaye
May 11, 2020 22:11Spika wa bunge la Libya amebainisha kwamba, serikali ya Tripoli haimtambui Jenerali Khalifa Haftar kuwa mshirika wake wa kisiasa wa baadaye.
-
Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya: Tumekiharibu kikamilifu kituo cha anga cha Haftar
May 11, 2020 03:38Serikali ya Mwafaka wa Kitaifa ya Libya (GNA) imetangaza kuwa, mashambulio ya anga yaliyofanywa na vikosi vyake yamekiharibu kikamilifu kituo cha anga cha vikosi vinavyoongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar.
-
Tunisia yaisaidia Uturuki kufikisha misaada Libya
May 08, 2020 19:30Serikali ya Tunisia imeiruhusu ndege ya Uturuki ambayo inasemekana ilikuwa na misaada ya kitiba kwa ajili ya Libyan itue nchini humo.