-
Wanamgambo wa Haftar wafanya mashambulio makubwa dhidi ya mji mkuu Tripoli
Apr 18, 2020 03:23Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya imetangaza kuwa, wanamgambo wanaoongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar wamefanya mashambulio makubwa dhidi ya mji mkuu wa nchi hiyo Tripoli.
-
Misri, Saudia na UAE zaandaa mkakati mpya kuliokoa kundi la Haftar lisisambaratishwe katika vita vya Libya
Apr 16, 2020 10:09Sambamba na kushindwa mtawalia kundi liitwalo Jeshi la Taifa la Libya (LNA) katika hujuma na mashambulio linayofanya ya kutaka kuudhibiti mji mkuu wa nchi hiyo, Tripoli, Misri, Saudi Arabia na Imarati (UAE) zimefikia makubaliano ya kuwapatia misaada zaidi wapiganaji wa kundi hilo.
-
Mamia ya wafungwa watoroka jela nchini Libya
Apr 16, 2020 03:20Mamia ya wafungwa waliokuwa wamefungwa jela katika mji wa Surman wa magharibi mwa mji mkuu wa Libya, Tripoli, wametoroka jela na kukimbilia kusikojulikana.
-
Kushadidi vita nchini Libya katika kivuli cha virusi vya Corona
Apr 14, 2020 06:43Licha ya kuibuka virusi vya Corona na kuenea kote ulimwenguni na hilo kupelekea kusitishwa vita na mapigano katika maeneo mengi ya dunia, lakini nchini Libya kwa sasa vita vimeshika kasi.
-
Vikosi vya serikali ya Libya vyakomboa miji minane iliyokuwa ikishikiliwa na wapiganaji wa Haftar
Apr 14, 2020 03:18Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa ya Libya (GNA) imetangaza kuwa vikosi vyake vimekomboa miji minane iliyokuwa ikidhibitiwa na wapiganaji watiifu kwa jenerali muasi Khalifa Haftar.
-
Wanamgambo 1,500 wa Kisyria wawasili Libya kushirikiana na Haftar
Apr 13, 2020 05:35Vikosi vya jeshi la Khalifa Haftar vimetangaza kuwa wanamgambo 1,500 wa Kisyria wamewasili Tripoli wakisaidiwa na Uturuki.
-
UAE yanunua mfumo wa makombora wa Israel na kuwapa wapiganaji wa Haftar
Apr 12, 2020 23:08Umoja wa Falme za Kiarabu umenunua mfumo wa kisasa wa makombora kutoka utawala wa Kizayuni wa Israel, kwa ajili ya kuwapa wanamgambo wa kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar.
-
Mapigano yaendelea kushuhudiwa Libya baina ya vikosi vya serikali ya Fayez al-Sarraj na wanamgambo wa Haftar
Apr 12, 2020 07:43Mapigano makali yanaripotiwa kuendelea nchini Libya baina ya vikosi vya Serikali ya Maafikiano ya Kitaifa inayoongozwa na Fayez al-Sarraj na wanamgambo watiifu kwa jenerali muasi Khalifa Haftar.
-
Vikosi vya Haftar vyafanya hujuma ya kukata umeme katika mji mkuu wa Libya, Tripoli
Apr 10, 2020 23:45Vikosi vya kundi linalojiita Jeshi la Taifa la Libya (LNA) linaloongozwa na jenerali muasi Khalifa Haftar vimefanya hujuma ya kusababisha umeme kukatika katika baadhi ya maeneo ya mji mkuu wa Libya, Tripoli.
-
Vikosi vya Haftar vyadai vimetungua drone 2 za Uturuki huko Libya
Apr 09, 2020 03:51Kundi la wanamgambo wanaojiita Jeshi la Tifa la Libya wanaoongozwa na jenerali Khalifa Haftar linadai kuwa limetungua ndege mbili zisizo na rubani za Uturuki zilizokuwa zikiruka katika anga ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika.