-
Wananchi wa Senegal waandamana kulaani ubaguzi wa rangi Marekani
Jun 11, 2020 08:04Wananchi wa Senegal wamefanya maandamano kulaani ubaguzi wa rangi na ukatili wa polisi ya Marekani dhidi ya raia weusi wa nchi hiyo.
-
Njama mpya nchini Lebanon; fitina za kimadhehebu kwa mbinu za kisiasa
Jun 10, 2020 13:29Katika siku za karibuni Lebanon kwa mara nyingine imekuwa ikishuhudia machafuko ambapo watu wa kushukiwa na kutiliwa shaka wamekuwa wakimiminika mitaani na kupiga nara za kichochezi na za fitiza za kimadhehebu pamoja na kukabiliana na walinda amani nchini humo.
-
Wananchi wa Kenya waandamana kulaani ukatili wa polisi ya nchi hiyo
Jun 09, 2020 08:06Wananchi wa Kenya wamefanya maandamano katika mji mkuu Nairobi, kulaani ukandamizaji na ukatili wa polisi ya nchi hiyo dhidi ya raia.
-
Wapalestina waandamana dhidi ya utawala wa Kizayuni katika Ukingo wa Magharibi
Jun 09, 2020 03:44Makumi ya Wapalestina wanaoishi katika mji wa Ramallah katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan wameandamana kupinga mpango wa utawala wa Kizayuni ambao unalenga kuteka ardhi zaidi za Wapalestina katika eneo hilo.
-
Wakazi wa New York waendeleza maandamano ya kupinga ubaguzi wa rangi nchini Marekani
Jun 06, 2020 17:16Wakazi wa New York nchini Marekani wameendeleza maandamano ya kupinga ubaguzi na ukatili wa polisi ya nchi hiyo dhidi ya watu weusi.
-
Maandamano ya kulaani ukatili wa polisi ya Marekani yafanyika Kenya, Nigeria
Jun 03, 2020 03:56Miji mikuu ya Kenya na Nigeria jana ilishuhudia maandamano ya kulaani ubaguzi wa rangi na mauaji ya George Floyd, raia wa Marekani mwenye asili ya Afrika aliyeuliwa kikatili na polisi mmoja mzungu katika mji wa Minneapolis, katika jimbo la Minnesota nchini Marekani wiki iliyopita.
-
Rais wa Ghana: Natumai mauaji ya Floyd yatachochea mabadiliko Marekani
Jun 03, 2020 03:55Rais wa Ghana ameashiria kuhusu mauaji ya kutisha ya Mmarekani mmoja mwenye asili ya Afrika katika mji wa Minneapolis nchini Marekani na kusema kuwa, "natumai kifo cha George Floyd kitakuwa chachu ya madiliko ya kudumu ya matatizo ya chuki na ubaguzi."
-
Maandamano ya kulaani ubaguzi wa rangi na ukatili wa polisi ya Marekani yasambaa duniani kote
Jun 01, 2020 10:25Maandamano ya kulaani ubaguzi wa rangi na jinai ya polisi mweupe kumuuua Mmarekani mwenye asili ya Afrika sambamba na kuendelea kushuhudiwa katika miji na majimbo mbalimbali ya Marekani, lakini pia yamesambaa na kuenea kwa kasi katika nchi mbalimbali duniani hususan za Ulaya.
-
Maandamano, ghasia zashtadi Marekani licha ya 'kafyu' na kamatakamata
May 31, 2020 11:46Licha ya agizo la kutotoka nje usiku na kukamatwa mamia ya waandamanaji, lakini maandamano ya kulaani ubaguzi wa rangi na jinai ya polisi mweupe kumuuua Mmarekani mwenye asili ya Afrika, yameendelea kushuhudiwa katika miji na majimbo mbalimbali ya Marekani.
-
Iran: Sauti ya waandamanaji nchini Marekani lazima isikilizwe
May 30, 2020 08:15Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran sanjari na kulaani mauaji ya raia wa Marekani wenye asili ya Afrika, imesisitiza kuwa sauti za watu wanaoandamana kulaani ukatili wa polisi ya nchi hiyo dhidi ya watu weusi lazima isikilizwe.