-
Kufichuliwa hitilafu kati ya Berlin na Washington kuhusu Ukraine
Jan 29, 2022 23:08Gazeti la Ishpigel la nchini Ujerumani limeripoti kuwa Emily Haber Balozi wa Ujerumani mjini Washington ametuma barua ya siri kwa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Ujerumani akisistiza kuwa Washington inaitambua Ujerumani kama nchi muitifaki asiyeaminika kutokana na kushindwa kutoa ushirikiano unaohitajika kuhusu kadhia ya Ukraine.
-
Takwa la Russia kwa ajili ya kuondoka haraka vikosi vamizi ajinabi huko Syria
Jan 29, 2022 08:46Dmitry Polyanskiy Naibu Mwakilishi wa Russia katika Umoja wa Mataifa amesema katika hotuba yake katika kikao cha Baraza la Usalama la umoja huo kuwa Russia inataka kuondoka haraka iwezekanavyo vikosi vyote vamizi ajinabi ambavyo vipo kinyume cha sheria huko Syria.
-
New York Times: Israel imekuwa ikitumia programu ya kijasusi ya Pegasus kupeleka mbele malengo yake
Jan 29, 2022 07:26Gazeti la The New York Times la Marekani limefichua kuwa, utawala wa Kizayuni wa Israel umetumia programu ya kijasusi ya "Pegasus" kuendeleza siasa zake za uhasama.
-
Khatami: Vikwazo vyote vya Marekani dhidi Iran lazima viondolewe
Jan 28, 2022 07:24Imam wa muda wa Sala ya Ijumaa ya hapa mjini Tehran amegusia mazungumzo yanayoendelea mjini Vienna kuhusu kuondolewa vikwazo vya kidhulma ilivyowekewa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na kusema kuwa, Marekani ina wajibu wa kuondoa vikwazo vyote ilivyoiwekea Iran, tena kwa sura ya kudumu.
-
Amnesty International: Jinai ya Saudia kwenye jela ya Saada imefanyika kwa silaha za Marekani
Jan 27, 2022 23:33Shirika la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesisitiza kuwa, mauaji ya jela ya Saada nchini Yemen yalitekelezwa kwa silaha za Marekani kufuatia mashambulizi ya muungano vamizi wa Saudi Arabia.
-
Vyombo vya habari vya Russia: Marekani na Uingereza zinaiuzia Ukraine silaha zilizochakaa
Jan 27, 2022 22:09Vyombo vya habari vya Russia vimeripoti kuwa, Marekani na Uingereza zinaiuzia Ukraine silaha na zana za kijeshi zilizochakaa na za zamani sana.
-
Askari aliyepindua serikali ya Burkina Faso alipata mafunzo Marekani
Jan 27, 2022 06:52Afisa wa kijeshi aliyeoongoza mapinduzi yaliyopelekea kupinduliwa rais aliyechaguliwa kidemokrasia Burkina Faso alipata mafunzo yake Marekani.
-
Marekani yaendelea kuiuzia Misri silaha licha ya faili lake jeusi la haki za binadamu
Jan 26, 2022 23:07Marekani imeidhinisha mauzo ya silaha zenye thamani ya dola bilioni 2.5 kwa Misri licha ya serikali ya nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika kuendelea kuandamwa na shutuma za ukiukaji wa haki za binadamu.
-
Mazungumzo ya Vienna; ufunguo wa makubaliano yoyote ni kuondolewa vikwazo vya kidhalimu dhidi ya taifa la Iran
Jan 26, 2022 23:05Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Sayyid Ebrahim Raisi ameeleza kuwa, ufunguo wa mapatano yoyote ya kuhuisha mapatano ya nyuklia ya JCPOA ni kuondolewa vikwazo vya kidhalimu dhidi ya wananchi wa Iran.
-
Iran: Hatujaamua kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na Marekani
Jan 25, 2022 04:35Waziri wa Mashauri ya Kigeni ya Iran amesema Jamhuri ya Kiislamu haijafikia uamuzi wa kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na Marekani.