-
Kugonga mwamba njama ya Marekani UN ya kupitisha azimio la kulaani Muqawama wa Palestina
Jun 02, 2018 22:10Rasimu ya azimio lililopendekezwa na Marekani, la kuuunga mkono utawala wa Kizayuni wa Israel na kulaani makundi ya muqawama wa Palestina imekataliwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
-
Mgogoro wa Marekani na Rwanda kuhusu nguo za mtumba
Jun 02, 2018 08:53Hatua ya serikali ya Rwanda kupiga marufuku nguo za mtumba kutoka Marekani imepelekea kuibuka msuguano baina ya nchi hizo mbili.
-
US yatumia veto kupinga azimio la kutaka kulindwa Wapalestina
Jun 02, 2018 03:18Marekani imetumia kura yake ya turufu kupinga rasimu ya azimio iliyowasilishwa na Kuwait katika Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, ikitaka kulindwa Wapalestina katika Ukanda wa Ghaza na Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu.
-
Sisitizo la Bashar Asad la kuondoka askari wa Marekani katika ardhi ya Syria
Jun 01, 2018 23:25Akizungumza hapo siku ya Alkhamisi na televisheni ya Rusia al-Yaum, Rais Bashar Asad wa Syria ameashiria nafasi hasi na ya kichochezi ya Marekani katika mgogoro wa nchi hiyo na kutaka askari wake waondoke mara moja katika ardhi ya nchi hiyo.
-
Kuanza vita vya kibiashara kati ya Trump na washirika wake wakuu wa kibiashara
Jun 01, 2018 09:07Hatimaye Rais Donald Trump wa Marekani ameanza kutekeleza kivitendo vita vya kibiashara kati ya nchi hiyo na washirika wake wa Ulaya kwa kuziwekea ushuru mpya bidhaa za chuma cha pua na alumini (aluminiamu) zinazoingizwa nchini humo kutoka nje.
-
Muungano wa kijeshi wa Marekani wakiri kuua raia 892 wa Syria na Iraq
Jun 01, 2018 03:13Muungano wa kimataifa unaoongozwa na Marekani wa eti kupambana na kundi la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) umekiri kupitia ripoti uliyotoa hapo jana kuwa tangu yalipoanza mashambulio ya anga ya muungano huo mwaka 2014 hadi sasa raia 892 wameuawa katika nchi za Syria na Iraq.
-
Larijani: Tatizo la Marekani ni kusimama kidete taifa la Iran kukabiliana na Uistikbari
May 31, 2018 22:32Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran amesema tatizo la Marekani ni kusimama imara taifa la Iran kukabiliana na Uistikabri na akafafanua kwa kusema: Marekani na waitifaki wake wanataka kuunda makundi ya kigaidi katika eneo la Magharibi ya Asia ili kuhatarisha usalama wa Iran.
-
Askofu Mkuu wa Iran: Marekani haina uwezo wa kukabiliana na mshikamano wa taifa la Iran
May 31, 2018 20:26Askofu Mkuu wa Wakristo wa Kiarmenia wa Tehran na kaskazini mwa Iran amesema kuwa, karibu miaka 40 sasa taifa la Iran limesimama imara kukabiliana na vikwazo kwa nguvu zake zote hivyo, Marekani na mabeberu wengine wa dunia hawana uwezo wa kukabiliana na umoja na mshikamano wa taifa la Iran.
-
Kuendelea vikwazo; kilele cha uadui wa Marekani dhidi ya Iran
May 31, 2018 20:22Vikwazo vipya vimetangazwa dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kufuatia uamuzi wa Marekani wa kujitoa katika makubaliano ya nyuklia ya Mpango Kamili wa Pamoja wa Utekelezaji JCPOA.
-
Qassemi: Marekani inatumia vibaya dini kuzusha ugomvi katika baadhi ya mataifa
May 31, 2018 10:29Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amejibu ripoti iliyotolewa na wizara ya mambo ya nje ya Marekani kuhusu uhuru wa kidini duniani na kusema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaiona ripoti hiyo kuwa haikuzingatia ukweli wa mambo, haina mashiko wala msingi wowote bali imetolewa kwa malengo ya kiuadui na kwa shabaha ya kutumia vibaya dini kwa malengo ya kisiasa.