-
Khatami: Fujo za Iran zimechochewa na Marekani na waitifaki wake
Jan 05, 2018 11:45Khatibu wa Sala ya Ijumaa iliyosaliwa leo hapa mjini Tehran amesema, fujo ambazo zimeshuhudiwa siku za hivi karibuni mjini Tehran zinaashiria kuwepo uchochezi wa Marekani na vibaraka wake.
-
Sisitizo la Lebanon kwa nchi za Kiarabu la kuishinikiza kidiplomasia Marekani
Jan 05, 2018 04:44Kufuatia uamuzi wa Rais Donald Trump wa Marekkani dhidi ya Beitul-Muqaddas, Spika wa Bunge la Lebanon amesisitiza juu ya ulazima wa kufungwa balozi za nchi za Kiarabu nchini Marekani.
-
Macron: Vitisho vya US, Israel na Saudia dhidi ya Iran ni njia ya vita
Jan 04, 2018 04:23Rais Emmanuel Macron wa Ufaransa ametaka kulindwa njia ya mazungumzo na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
-
Rouhani na Erdogan walaani msimamo wa US, Israel dhidi ya Iran
Jan 03, 2018 23:05Marais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Uturuki wamekosoa vikali uchochezi na uungaji mkono wa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel kwa waandamanaji wanaofanya fujo na ghasia nchini.
-
Gaidi wa Boko Haram ajiripua na kuua watu 14 msikitini nchini Nigeria
Jan 03, 2018 12:03Mtu aliyejifunga bomu mwilini amejiripua na kuua watu wasiopungua 14 ndani ya msikiti mmoja katika mji wa Gamboru ulioko kwenye jimbo la Borno, kaskazini mashariki mwa Nigeria leo.
-
Jibu la Wapakistan kwa matamshi mapya ya Trump
Jan 03, 2018 09:46Matamshi mapya ya Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu makosa ya kistratijia ya nchi hiyo katika kuipa Pakistan misaada ya kifedha kwa zaidi ya muongo mmoja uliopita, yamekabiliwa na radiamali kali kutoka kwa Wapakistan.
-
Ripoti: Trump amesema uwongo mara elfu 2 ndani ya siku 347
Jan 02, 2018 11:25Ripoti mpya iliyochapishwa na gazeti la The Washington Post imesema Rais Donald Trump wa Marekani amesema urongo karibu mara elfu mbili ndani ya siku 347 alizohudumu ndani ya Ikulu ya White House.
-
Viongozi wa kisiasa Pakistan wakerwa na Trump, waitaka serikali kuisusa US
Jan 02, 2018 04:21Viongozi wa vyama vya siasa na wanaharakati nchini Pakistan wameonyesha kukerwa mno na matamshi ya Rais Donald Trump wa Marekani kuhusu nchi yao.
-
Iran: Kabla ya Trump kuingilia Iran, aokoe kwanza mamilioni ya Wamarekani wanaokufa njaa
Jan 02, 2018 04:15Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Uingereza amejibu uingiliaji wa Rais Donald Trump wa Marekani katika masuala ya ndani ya Iran na kusema kuwa, licha ya Marekni kujulikana kuwa na uwezo mkubwa wa kiuchumi duniani, lakini kwa mwaka idadi kubwa ya raia wake huwa wanakufa njaa kutokana na tofauti ya kitabaka.
-
Shamkhani: Marekani, Uingereza na Saudia zapokezana mashambulizi ya Intaneti dhidi ya Iran
Jan 02, 2018 01:14Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran amesema kuwa, Marekani, Uingereza na Saudi Arabia zimeanzisha vita vya kupokezana katika Intaneti kuishambulia kila upande Jamhuri ya Kiislamu na taifa la Iran.