-
Russia: Stratejia mpya ya US nchini Afghanistan, hatima isiyo na tija
Aug 24, 2017 09:49Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Russia amesema stratejia mpya ya kijeshi ya Washington kuhusiana na Afghanistan itagonga mwamba kwa kuwa inasisitizia utumiaji wa mabavu.
-
Misri yalalamikia hatua ya Marekani ya kuikatia misaada
Aug 24, 2017 09:22Serikali ya Misri imekosoa vikali hatua ya Marekani ya kuikatia misaada nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika na kutahadharisha juu ya taathira hasi inayoikodolea macho Washington kutokana na kitendo chake hicho.
-
Stratijia mpya ya kijeshi ya Marekani nchini Afghanistan
Aug 23, 2017 07:22Hatimaye baada ya miezi kadhaa ya mizozano katika timu ya usalama wa taifa ya Marekani, siku ya Jumatatu iliyopita Rais wa nchi hiyo Donald Trump, alitangaza stratijia mpya ya vita ya Washington kuhusiana na Afghanistan sambamba na mpango wa kutuma askari zaidi nchini humo.
-
NATO yaunga mkono stratejia mpya ya Marekani kuhusu Afghanistan
Aug 22, 2017 23:12Muungano wa Kijeshi wa NATO umeunga mkono uamuzi wa Rais wa Marekani wa kuongeza wanajeshi wengine nchini Afghanistan katika kalibu ya stratejia mpya ya Washington.
-
Malengo ya safari ya Waziri wa Ulinzi wa Marekani katika nchi za Jordan, Uturuki na Ukraine
Aug 21, 2017 03:44Waziri wa Ulinzi wa Marekani, James Mattis jana Jumapili aliwasili Amman katika awamu ya kwanza ya safari ya kuzitembelea nchi tatu za Jordan, Uturuki an Ukraine.
-
China yazalisha kombora la mabara aina ya Julang-3, kujiandaa na vita na Marekani
Aug 20, 2017 12:05Katika kuongeza uwezo wa kijeshi, serikali ya China imeendelea kuzalisha na kustawisha kombora la mabara la kizazi kipya kwa jina la Julang-3, ambalo limetajwa kuwa ni maandalizi ya kuingia katika vita tarajiwa na Marekani.
-
Korea Kaskazini: Chokochoko za Marekani zikiongezeka, tutaishambulia bila huruma
Aug 20, 2017 12:00Kwa mara nyingine serikali ya Korea Kaskazini imetoa onyo kali kwa Marekani kwa kusema kuwa, ikiwa siasa za uhasama na kupenda kujitanua dhidi ya Pyongyang zitaendelea na hatimaye kuisukuma nchi hiyo kuingia katika vita vya nyuklia, basi Washington itakabiliwa na mashambulizi makali.
-
Ayatullah Araki: Iran imesambaratisha njama zote za Marekani Iraq, Palestina, Yemen na Syria
Aug 18, 2017 03:38Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kukurubisha Pamoja Madhehebu za Kiislamu amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesambaratisha njama za Marekani nchini Iraq, Palestina, Yemen na Syria.
-
Mwanastratijia wa Trump: Mgogoro wa Korea Kaskazini hauna njia ya utatuzi wa kijeshi
Aug 17, 2017 23:36Mwanastratijia wa ngazi ya juu wa ikulu ya Marekani (White House) ametoa matamshi yanayopingana na vitisho vya Rais Donald Trump wa nchi hiyo dhidi ya Pyongyang na kusema kuwa, suala la Korea Kaskazini halina njia ya utatuzi wa kijeshi.
-
Katibu Mkuu wa UN akerwa na vita vya maneno kati ya US na Korea Kaskazini
Aug 17, 2017 03:12Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ameeleza wasiwasi wake kuhusu kushtadi vita vya maneno kati ya Marekani na Korea Kaskazini na kusema kuwa, kuna haja ya pande mbili hizo kukumbatia diplomasia.