-
Mkutano kuhusu Libya nchini Marekani wafutwa kutokana na amri ya Trump
Feb 04, 2017 04:27Mkutano kuhusu Libya uliokuwa umepangwa kufanyika nchini Marekani tarehe 16 mwezi huu umefutwa kutokana amri ya rais Donald Trump ya kupiga marufuku raia wa nchi saba za Kiislamu ikiwemo Libya kuingia nchini humo.
-
Madai ya Trump kuhusu kuanza sera mpya za kigeni za Marekani
Feb 02, 2017 08:18Rais Donald Trump wa Marekani, akizungumza katika sherehe za kuapishwa Rex W. Tillerson kama waziri mpya wa mambo ya nje wa nchi hiyo, amesema wakati umefika kwa sera za kigeni kusimamiwa na mtu mwenye macho ya wazi ili aweze kuutazama ulimwengu kwa macho mapya kwa lengo la usuluhishaji wenye kuzingatia ukweli wa kale.
-
Trump atishia kuwa Marekani itaishambulia kijeshi Mexico
Feb 02, 2017 03:52Rais wa Marekani Donald Trump ametishia kutuma vikosi vya jeshi la nchi hiyo nchini Mexico.
-
Hatua mpya ya uungaji mkono wa Marekani kwa makundi ya kigaidi katika serikali ya Trump
Feb 01, 2017 23:20Licha ya kuwepo indhari mbalimbali juu ya uwezekano wa Marekani kuyapatia makundi ya kigaidi msaada wa silaha, serikali ya Rais Donald Trump imelitumia silaha kundi moja la wabeba silaha nchini Syria.
-
Rouhani: Uongo wa madai ya Marekani ya kuwaunga mkono wananchi wa Iran umethibitika
Feb 01, 2017 13:05Rais Hassan Rouhani amesema kuwabatilishia viza raia wa mataifa mengine ni hatua inayochukuliwa na watu wanagenzi katika ulingo wa siasa na kusisitiza kwamba uamuzi mpya uliopitishwa na serikali ya Marekani umethibitisha kuwa madai yake ya kuwaunga mkono wananchi wa Iran ni uongo mtupu.
-
Maandamano dhidi ya ubaguzi wa Trump yapamba moto US
Feb 01, 2017 04:19Maelfu ya watu pasina kujali dini na rangi zao wameshadidisha maandamano katika kona mbali mbali za Marekani, kulaani sheria tata ya ubaguzi iliyopasishwa na Rais Donald Trump wa nchi hiyo hivi karibuni.
-
Iran kuitupa sarafu ya dola baada ya maamuzi ya kibaguzi ya Trump
Feb 01, 2017 00:51Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema inapanga kuacha kutumia sarafu ya dola katika taarifa rasmi za kifedha kufuatia hatua ya wakuu wa Washington kuiweka nchi hii katika orodha ya nchi saba ambazo raia wake wanazuiwa kuingia Marekani.
-
Sudan yakosoa sheria ya kibaguzi ya Trump dhidi ya Waislamu
Jan 31, 2017 10:15Msuguano wa kidiplomasia kati ya Washington na Khartoum umeibuka tena baada ya Rais wa Marekani Donald Trump kupasisha sheria ya kuzuia raia wa Sudan na nchi nyingine 6 za Kiislamu kuingia nchini Marekani.
-
Iraq yajibu mapigo, Bunge lapasisha sheria ya kuwazuia Wamarekani kuingia nchini humo
Jan 31, 2017 00:41Bunge la Iraq limejibu hatua ya serikali ya Rais Donald Trump wa Marekani ya kuwazuia Waislamu kuingia nchini humo kwa kupasisha sharia inayowapiga marufuku Wamarekani kuingia nchini Iraq.
-
Kuongezeka chuki dhidi ya Waislamu Amerika Kaskazini
Jan 31, 2017 00:39Baada ya kuongezeka hisia za chuki na uadui dhidi ya Waislamu huko Amerika Kaskazini hususan baada ya kuingia madarakani Rais Donald Trump nchini Marekani, hivi sasa matokeo mabaya ya jambo hilo yameanza kuonekana.