-
Trump asisitiza udharura wa kuimarishwa uwezo wa silaha za nyuklia wa Marekani
Dec 24, 2016 03:59Rais mteule wa Marekani, Donald Trump Alkhamisi ya jana alitangaza kuwa, nchi hiyo inapaswa kuimarisha zaidi uwezo wake wa silaha za nyuklia maadamu ulimwengu haujapata mwelekeo wa kimantiki kuhusu silaha za atomiki.
-
Jeshi la Marekani lahitimisha rasmi operesheni zake Sirte, Libya
Dec 21, 2016 11:15Jeshi la Marekani limetamatisha rasmi operesheni zake katika mji wa pwani wa Sirte nchini Libya, ambao hivi karibuni ulikombolewa kikamilifu toka mikononi mwa magaidi wa Daesh.
-
Yahya Jammeh: Siondoki madarakani; hakuna wa kuniondoa isipokuwa Mwenyezi Mungu
Dec 21, 2016 03:38Rais Yahya Jamme ambaye alishindwa katika uchaguzi wa mwanzoni mwa mwezi huu amesisitiza kwamba, hataachia ngazi na kuondoka madarakani.
-
Ja'fari akosoa njama zinazofanywa na nchi za Magharibi nchini Syria
Dec 21, 2016 00:22Mwalikishi wa kudumu wa Syria katika Umoja wa Mataifa amekosoa njama zinazofanywa na Marekani, Uingereza na Ufaransa kwa ajili ya kuingilia mambo ya ndani ya Syria.
-
Saudia: Marekani haijapunguza mauzo ya silaha zake kwetu
Dec 19, 2016 04:04Adel al-Jubeir, Waziri wa Mambo ya Nje wa Saudi Arabia amekanusha madai kuwa Marekani imepunguza kiwango cha uuzaji silaha kwa serikali ya Riyadh kutokana na hujuma za utawala huo wa kifalme nchini Yemen.
-
Harakati ya Ansarullah ya Yemen: Marekani na Israel ndio maadui wa Umma wa Kiislamu
Dec 17, 2016 13:12Serikali ya Wokovu wa Kitaifa ya Yemen imesisitiza juu ya udharura wa kutumiwa mafundisho ya Bwana Mtume (saw) kwa ajili ya kukabiliana na Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel tawala mbazo ni maadui wa Umma wa Kiislamu.
-
Wito wa Mogherini wa kutaka EU na Russia ziwe na msimamo mmoja kuhusiana na JCPOA
Dec 17, 2016 03:43Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya ametaka kuwepo na msimamo mmoja baina ya umoja huo na Russia katika kuunga mkono makubaliano ya nyuklia ya JCPOA na kukabiliana na hatua yoyote ya kukwamisha utekelezaji wa makubaliano hayo.
-
Vifo vinavyotokana na utumiaji mihadarati na pombe Marekani vimeongezeka mara tatu
Dec 17, 2016 00:53Watafiti wa elimu ya tiba nchini Marekani wametangaza kuwa uchunguzi waliofanya katika maeneo 3,100 ya nchi hiyo unaonesha kuwa tangu mwaka 1980 hadi sasa idadi ya Wamarekani wanaofariki kutokana na utumiaji madawa ya kulevya, pombe na maradhi yanayotokana na matatizo ya akili imeongezeka mara tatu.
-
Trump ateua Mzayuni mwenye misimamo mikali kuwa balozi wa US, Israel
Dec 16, 2016 04:47Rais mteule wa Marekani ameteua David Friedman, Mzayuni mwenye misimamo ya kuchupa mipaka kuwa balozi wa Marekani katika utawala haramu wa Israel.
-
Russia: Madai kuwa Putin aliingilia uchaguzi wa Marekani ni 'dhihaka'
Dec 16, 2016 04:46Msemaji wa Ikulu ya Russia (Kremlin) amesema madai yanayoenezwa na vyombo vya habari kuwa Rais Vladimir Putin wa nchi hiyo aliingilia uchaguzi wa Marekani ni 'dhihaka' na madai ya upuuzi.