Mar 22, 2016 06:54
Huku wiki moja ikiwa imepita katika muda uliowekwa wa siku 10 kwa ajili ya mazungumzo ya amani ya Syria yanayofanyika mjini Geneva, hadi sasa hakuna chochote kilichoibuka kutoka ndani ya mazungumzo hayo, bali kwa mara nyengine tena wingu la hitilafu limetanda kwenye anga ya mazungumzo baina ya pande mbili husika.