Misikiti kadhaa mjini London Uingereza imepokea vitisho vya kigaidi kutoka kwa makundi yanayoaminika kuwa ya wabaguzi wa mrengo wa kulia huku vitendo vya chuki dhidi ya Uislamu vikiongezeka nchini humo.
Watu wanane wameuawa na wengine kadhaa kujeruhiwa katika shambulio lililofanywa msikitini na watu waliokuwa na silaha katika mji wa al Junaynah mkoani Darfur Magharibi huko Sudan.
Genge la watu waliouhujumu msikiti mmoja wa mjini Mwanza kaskazini mwa Tanzania Jumatano usiku na kutekeleza mauaji walikuwa na bendera za kundi la kigaidi la ISIS au Daesh.
Watu wawili wameuawa na wengine 15 wamejeruhiwa wakati ulipotokea mripuko ndani ya msikiti katika mji wa Beledweyne mkoani Hiiraan katikati mwa Somalia hapo jana.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa amelaani vikali shambulizi la kigaidi lililolenga msikiti nchini Nigeria na kuua watu 25.