Mar 06, 2024 03:37
Wataalamu wa masuala ya kijeshi wamesema, baada ya kupita siku 150, utawala wa Kizayuni wa Israel haujaweza kufikia malengo uliyotangaza kuwa sababu ya kuanzisha vita dhidi ya Ukanda wa Ghaza, licha ya kuua maelfu ya Wapalestina, kujeruhi maelfu ya wengine, mbali na mamia ya maelfu walioachwa bila makazi pamoja na kuugeuza ukanda huo kuwa eneo la magofu.