-
Takwa la Pakistan kwa Taliban la kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na serikali ya Afghanistan
Jan 12, 2019 23:26Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Pakistan amelitaka kundi la wanamgambo wa Taliban kufanya mazungumzo ya moja kwa moja na serikali ya Afghanistan bila ya kupitia kwa mtu mwingine ili kufanikisha malengo ya amani.
-
Jibu la Pakistan kwa matamshi ya hivi karibuni ya Waziri Mkuu wa India
Jan 04, 2019 04:33Msemaji wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Pakistan amelaani vikali vitisho na matamshi yaliyotolewa hivi karibuni ya Waziri Mkuu wa India dhidi ya Pakistan.
-
Sisitizo la maulamaa wa Pakistan la kuwa kitu kimoja Waislamu wa Kishia na Kisuni
Dec 22, 2018 21:36Maulamaa wa Kishia na Kisuni wa Pakistan wametilia mkazo kuwepo umoja kati ya Waislamu nchini humo ili kukabiliana na njama za maadui wa Uislamu.
-
Rouhani: Madola ya kibeberu ndiyo yaliyounda makundi ya kigaidi duniani
Dec 09, 2018 00:05Rais Hassan Rouhani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema madola ya kibeberu ndiyo yaliyounda na kuyafadhili kwa hali na mali makundi ya kigaidi duniani, na kwamba irada thabiti na jitihada za pamoja zinahitajika ili kulitokomeza jinamizi hilo linalotishia usalama wa dunia.
-
Mkutano wa maspika wa mabunge ya nchi sita wamalizika mjini Tehran kwa kutoa taarifa
Dec 08, 2018 12:07Maspika wa mabunge ya nchi sita za Iran, Russia, Uturuki, China, Pakistan na Afghanistan umemalizika leo hapa mjini Tehran kwa taarifa ya pamoja ya kuimarisha uhusiano katika kupambana na ugaidi na kuongeza ushirikiano wao wa kieneo.
-
Pakistan: Hatutaendelea kuwa kibaraka wa Marekani
Dec 07, 2018 11:03Waziri Mkuu wa Pakistan, Imran Khan ameeleza namna nchi hiyo inavyojuta kwa namna ilivyoamiliana vizuri na Marekani huko nyuma, akisisitiza kuwa Islamabad haitaendelea kuwa kibaraka wa Washington.
-
Kongamano la "Rehma kwa Walimwengu" latoa sisitizo kwa Waislamu kuhuisha Uislamu wa Asili
Nov 23, 2018 01:08Taarifa ya mwishoni mwa kongamano la siku mbili lililofanyika mjini Islamabad, Pakistan kwa anuani ya "Rehma kwa Walimwengu" limetoa sisitizo juu ya ulazima wa Waislamu duniani kushikamana na Uislamu wa asili kwa mujibu wa mafundisho ya Bwana Mtume Muhammad SAW.
-
Wapakistani waendelea kuandamana kupinga kuachiwa huru mwanamke aliyevunjia heshima matukufu ya Kiislamu
Nov 01, 2018 12:49Maelfu ya watu nchini Pakistan kwa siku ya pili mtawalia hii leo wamefanya maandamano katika miji mbalimbali ya nchi hiyo ukiwemo mji mkuu Islamabad wakilalamikia kuachiwa huru mwanamke mmoja raia wa nchi hiyo aliyeyavunjia heshima matukufu ya Kiislamu.
-
Utayari wa maulamaa wa Pakistan wa kusaidia mchakato wa amani nchini Afghanistan
Oct 07, 2018 03:27Maulamaa wa Pakistan wametangaza utayari wao wa kusaidia kuhitimisha vita nchini Afghanistan na kurejesha amani ya kudumu katika nchi hiyo.
-
Maulamaa wa Pakistan na Afghanistan wafikia mwafaka wa kufanya kikao cha pamoja ili kukomesha vita Afghanistan
Oct 04, 2018 04:50Maulamaa wa Pakistan na Afghanistan wamefikia mwafaka juu ya kufanya kikao cha pamoja kwa madhumuni ya kuhitimisha vita na mapigano nchini Afghanistan.