-
China yaitaka jamii ya kimataifa ishughulikie mgogoro wa Palestina
Aug 26, 2020 01:56Mwakilishi wa China katika Umoja wa Mataifa ametoa wito wa kupatikana suluhisho la mgogoro wa Palestina.
-
Shambulizi la anga la Israel laua shahidi Wapalestina 4 Gaza
Aug 25, 2020 03:28Wapalestina wanne wameuawa shahidi baada ya ndege za kivita za utawala wa Kizayuni wa Israel kushambulia kwa mabomu maeneo kadhaa ya Palestina huko mashariki mwa Ukanda wa Gaza.
-
Algeria: Kuitetea na kuiunga mkono Palestina ni katika sera zetu za nje
Aug 24, 2020 23:01Msemaji wa serikali ya Algeria amesema kusimama na wananchi wa Palestina, kuwatetea na kuwaunga mkono nio katika sera za nje zilizopewa kipaumbele na taifa hilo la Kiarabu la kaskazini mwa Afrika.
-
HAMAS yaomba mabunge na viongozi wa dunia waisaidie na kuiunga mkono Palestina
Aug 19, 2020 06:27Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS ameyataka mabunge duniani pamoja na viongozi wa kisiasa watoe msaada na uungaji mkono kwa kadhia ya Palestina kwa ajili ya kukabiliana na njama za utawala haramu wa Kizayuni wa Israel.
-
Uhusiano wa UAE na Israel unalenga kutoa pigo kwa Muqawama na malengo matukufu ya Palestina
Aug 17, 2020 08:46Kiongozi mwandamizi wa Harakati ya Muqawama wa Kiislamu ya Palestina HAMAS amesema, lengo la makubaliano yaliyofikiwa baina ya Imarati na utawala wa Kizayuni ni kutoa pigo la kuudhuru muqawama na malengo matukufu ya Palestina.
-
Harakati ya Kenya-Palestina yalaani mapatano ya UAE na Israel
Aug 16, 2020 02:16Harakati ya Mshikamano wa Kenya na Palestina imelaani vikali mapatano yaliyofikiwa baina ya watawala wa Umoja wa Falme za Kiarabu na utawala ghasibu wa Israel chini ya usimamizi wa makundi ya Kizayuni nchini Marekani.
-
Spika wa Bunge la Iran: Imarati imejidhalilisha kwa kuanzisha uhusiano na utawala wa Kizayuni
Aug 14, 2020 22:29Spika wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu (Bunge la Iran) amesema kuwa makubaliano ya Imarati na utawala wa Kizayuni wa Israel ya kuanzisha uhusiano baina ya pande hizo mbili ni ya kijidhalilisha na ni usaliti kwa thamani za Umma wa Kiislamu na malengo ya taifa la Palestina.
-
Palestina yamrejesha nyumbani balozi wake Abu Dhabi baada ya Imarati kuanzisha uhusiano na Israel
Aug 14, 2020 05:04Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Serikali ya Mamlaka ya Ndani ya Palestina ametangaza kuwa balozi wa Palestina mjini Abu Dhabi ameitwa nyumbani kulalamikia hatua ya Imarati ya kuanzisha rasmi uhusiano wa kidiplomasia na utawala haramu wa Israel.
-
Iran: Uhusiano wa kidiplomasia wa Abu Dhabi na Tel Aviv ni ujinga wa kistratijia
Aug 14, 2020 03:37Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran imelaani hatua ya kuanzishwa uhusiano wa kidiplomasia baina ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE au Imarati) na utawala wa Kizayuni wa Israel na kutaja hatua hiyo kuwa ni ujinga wa kistratijia ambao bila shaka utapelekea kuimarika mhimili wa muqawama na mapambano katika eneo.
-
Hamas: Wapalestina wanapaswa kuulinda Msikiti wa al Aqsa
Aug 11, 2020 02:14Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina (HAMAS) imewataka Wapalestina wote kutetea na kuulinda Msikiti mtakatifu wa al Aqsa na kukabiliana na njama za utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya msikiti huo.