-
Kamisheni: Israel imewakamata watoto 16,500 wa Kipalestina
May 26, 2019 23:52Ripoti mpya imefichua kuwa utawala wa Kizayuni wa Israel umewatia mbaroni watoto 16,500 tangu ilipoanza Intifadha ya Pili mwishoni mwa mwaka 2000.
-
Qatar: Amani ya Palestina sharti ijumuishe suluhu inayokubaliwa na Wapalestina
May 25, 2019 05:48Wizara ya Mambo ya Nje ya Qatar sambamba na kukosoa mpango wa kufanyika mkutano wa Marekani wa kuzindua hatua ya mwanzo ya utekelezaji wa 'Muamala wa Karne' mwezi ujao wa Juni nchini Bahrain, imesema matakwa ya wananchi wa Palestina lazima yajumuishe kwenye mipango yoyote ya amani na maendeleo inayowahusu.
-
Kufungwa UNRWA; takwa jipya la Marekani dhidi ya Palestina
May 24, 2019 00:11Rais Donald Trump wa Marekani alipoingia katika ikulu ya nchi hiyo White House, alichukua msimamo wa kuiunga mkono Israel bila ya masharti yoyote na wakati huo huo kudhihirisha uhasama wa waziwazi dhidi ya Wapalestina.
-
Waziri Mkuu wa Malaysia: Amani ya dunia inategemea amani ya Palestina
May 23, 2019 23:11Waziri Mkuu wa Malaysia, Mahathir Mohammed amesema iwapo dunia inataka kushuhudiwa amani endelevu, sharti kadhia ya Palestina ipatiwe ufumbuzi.
-
Palestina: Mkutano wa US nchini Bahrain ni wa kuboresha uhusiano wa Waarabu na Israel
May 22, 2019 03:39Harakati ya Jihad Islami ya Palestina imekosoa vikali mpango wa kufanyika mkutano wa Marekani wa kuzindua hatua ya mwanzo ya utekelezaji wa 'Muamala wa Karne' mwezi ujao wa Juni nchini Bahrain ikisisitiza kuwa kongamano hilo halina lengo jingine ghairi ya kuandaa mazingira ya kuimarisha na kufanya wa kawaida uhusiano kati ya Waarabu na utawala wa Kizayuni wa Israel.
-
Jordan yaombwa isishiriki mkutano wa Marekani nchini Bahrain
May 21, 2019 23:13Serikali ya Jordan imetakiwa kutoshiriki mkutano wa Marekani wenye lengo la kuzindua hatua ya mwanzo ya utekelezaji wa 'Muamala wa Karne' unaotazamiwa kufanyika mwezi ujao wa Juni nchini Bahrain.
-
Visa vya Wazayuni kuwagonga kwa gari Wapalestina kwa makusudi vyaongezeka
May 21, 2019 09:26Mlowezi wa Kizayuni amemgonga kwa gari Mpalestina kwa makusudi na kumuua shahidi katika Ukingo wa Magharibi wa Mto Jordan unaokaliwa kwa mabavu.
-
Riyadh al-Maliki: Mpango wa "Muamala wa Karne" ni sawa na kurejea katika ukoloni
May 18, 2019 20:50Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesema kuwa, kuukubali mpango wa amani wa Marekani katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu na utawala haramu wa Israel unaojulikana kama "Muamala wa Karne" ni kurejea katika kipindi cha ukoloni.
-
Iran: Israel ndiyo sababu ya migogoro yote ya kibinadamu Asia Magharibi
May 14, 2019 03:22Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imesema utawala wa Kizayuni wa Israel ndilo chimbuko la migogoro yote ya kibinadamu katika eneo la Asia Magharibi (Mashariki ya Kati).
-
Rais Mahmoud Abbas: Taifa la Palestina halitaukubali mpango wa 'Muamala wa Karne'
May 13, 2019 02:46Rais Mahmoud Abbas wa Mamlaka ya Ndani ya Palestina amesema kuwa, taifa la Palestina halitaukubali mpango wa Marekani wa 'Muamala ya Karne' kwa namna yoyote ile.